Brand sina neno zuri la Kiswahili lakini katika makala haya tutatafsiri kama ‘nembo’.Kimsingi ni alama ya biashara inayojumuisha rangi, alama, na vifupisho vya herufi. Nembo ikilindwa kisheria inaitwa ‘trade mark’. Katika taaluma ya biashara inaaminika kuwa bidhaa zinatambulika zaidi kwa nembo.
Hili linatokana na ukweli kwamba mteja mara zote anapata faraja ya ‘kisaikolojia’ mara anapotumia bidhaa anayoitambua kuliko kutumia bidhaa asiyoijua na jina au asiyoikubali kwa nembo ingawa inaweza kufanya vizuri.
Mfano mzuri wa jinsi akili zetu zinavyoweza kutekwa na uhimara wa nembo hadi kila kitu ukajikuta unakitambua kwa jina hilo ni nembo ya ‘Shell’, hii ni miongoni mwa kampuni kubwa ya mafuta duniani inayomilikiwa kwa ushirikiano wa Wadachi na Waingereza, lakini hadi leo katika Tanzania kila anayeenda katika kituo cha mafuta anatamka anakwenda Shell ingawa ukweli wa mambo ni kuwa Shell haipo katika biashara ya mafuta Tanzania.
Hili linaonesha wazi kuwa mteja anaponunua bidhaa mara nyingi hanunui bidhaa ananunua nembo.Kibiashara nembo inafaida nyingi, ikiwemo urahisi wa utambuzi kwa mlaji na kuhimarisha marudio ya matumizi.
Ingawa kwa sasa ulimwengu unashuhudia kuibuka kwa nembo binafsi (own brand) kwa kampuni nyingi kubwa duniani, lakini bado mauzo ya nembo zilizobuniwa na kampuni husika kama vile Lee, Levis, bado yapo juu.Katika Tanzania mageuzi haya pia yapo ndiyo tuna dangirizi za KP,Tippo, na vyakula vinavyofungwa kwa majina ya Supermarkets kama Shoprite. Moja ya kampuni kubwa inayofanya vizuri kwa kutumia nembo yake na si za wazalishaji ni Mark Spencer wenye nguo zinazokwenda kwa jina la kampuni badala kuwa nguo kama Lee, Levi’s kama tulivyozoea.
Nembo ni msingi wa biashara na ndiyo maana kuna kampuni zinachaji gharama kubwa si kwa tofauti ya malighafi tu ni kwa vile nembo yao iko na thamani kubwa na yenye kuheshimika. Wataalamu wa mambo ya fedha na mitaji wanakadiria kuwa asilimia 70 ya mtaji wa kampuni iko katika nembo.
Kwa mfano kampuni ya Zain Tanzania mwaka 2007 ilitumia zaidi ya bilioni 5. 1 za kitanzania kwa ajili ya matangazo ya nembo yake tu, hii kwa mujibu wa gazeti la Advertising Age, la Desemba 8 mwaka 2008.Mfano huu unatuonesha wazi kuwa mara nyingi kampuni zinawekeza katika kutangaza nembo zao.
Makala haya itajaribu kujadili umuhimu wa Tanzania kama nchi kupigania haki yake kutoka kwa kampuni za kimataifa au za ndani zinazotumia majina ya vivutio vyetu vya asili nasi tupate sehemu la pato kutokana na mauzo.
Katika Tanzania leo hii kuna makampuni mengi yanayotumia Kilimajanro, Serengeti, Mikumi na kadhalika kama sehemu ya nembo zao kibiashara. Takwimu haziko wazi kama Tanzania inanufaika kutokana na kampuni hizi kutumia majina yetu ya kijiografia kama nembo zao za kibiashara nchi inapata chochote.
Ila mfano wa Ethiopia inaonesha wazi kuwa nchi nyingi za Afrika zinakosa pato kubwa kutokana na matumizi ya nembo zao za kijiografia kutumika nasi hatulipwi hata shilingi.
Wakisaidiwa kisheria na Oxfam; Ethiopia ilichachamaa na kufungua madai ya haki miliki katika Ofisi za Haki Miliki nchini Marekani, ikiitaka Starbuck kampuni kubwa ya kimarekani kufikiria kuipa stahiki yake kwa kutumia nembo ya eneo moja katika Ethiopia kwa bidhaa zake za kahawa inayozalishwa na Starbuck.Kilio cha Ethiopia ilikuwa kudai pato linalotokana na chumo la 'premium price' linalovunwa na 'Starbuck' kutokana na kuuzwa kwa kahawa hiyo katika mikahawa mbalimbali inayomilikiwa na Starbuck katika Ulaya na Marekani.
Starbuck inatumia majina ya Sidamo, Harar na Yirgaeteffe maeneo katika Ethiopia kama nembo ya kahawa yake. Ikimbukwe kuwa Sidamo ni mahali ambako inaaminika ni moja kati ya sehemu ambazo mbegu ya kahawa ya kwanza ilioteshwa na binadamu, hivyo eneo hili inaonesha kuwa ni sehemu nzuri na ipo katika vichwa vya walaji makini wa kahawa na ni wazi kuwa wataithamini kahawa yenye jina hilo kwa heshima ya kihistoria.
Na ubora wa Sidamo kama eneo unatumika na Starbcuk katika matangazo yake kuinadi kahawa yake.Kahawa yenye nembo ya Sidamo ikiuzwa hadi dola 26 kwa kilo huku wakulima wa Ethiopia wakiambulia dola moja tu ya chumo.
Baada ya vuta ni kuvute iliyoanza tangu Mei 2005, Starbuck ilikubali kuipa Ethiopia dola milioni 88 kama pato linalotokana na kutumiwa kwa maeneo yake kama sehemu ya nembo ya biashara.Oxfam iliuita ushindi huu kama ‘fair trade’ ya aina yake kwani wakulima masikini wa Sidamo nao watapata chumo lingine toka kwa kutumika kwa nembo ya eneo lao.
Katika chapisho, Regional Branding Marketing, Matthew Muntberg, anataja sababu moja wapo ya kufanikiwa katika kuchagua jina zuri la nembo ya kijiografia ni kutafuta sehemu yenye heshima ya ‘kipekee’. Hivyo wanaotumia majina yetu ya kihistoria na urithi wa nchi yetu kama nembo zao kibiashara wanatambua hili kuwa ni vitu vyenye mvuto na kuheshimika.
Tanzania ina bidhaa ambazo zinatumia majina ya vivutio, kama vile mlima Kilimanjaro, Serengeti kwa mbuga ya wanyama yenye heshima kubwa Duniani. Bidhaa hizi ni kuanzia maji, bia na hoteli za kisasa zenye kutumia majina yetu ya kijiografia.
Aina ya nembo za maeneo (Regional /geographical Brand) si kitu kipya duniani, kuna Idaho Commission kakika Marekani yenye zaidi ya miaka 70, ikisimamia wazalishaji wanaotaka kutumia nembo hiyo ya eneo kwa kuzalisha viazi mbatata kulipa, huku ikijikusanyia zaidi ya dola milioni 12 kama kamisheni, ya kutumika kwa eneo lao kama nembo.
Kutoza watumiaji wa nembo za kijiografia ni chanzo kingine cha mapato kilicho sahaulika katika Tanzania. Na hili litatupunguzia kutoza kodi watu walio na hali duni hasa wakulima wa nchi hii kwa kodi ambazo ni za kidhalilishaji huku kuna vyanzo wenzetu wameviona na wanavitumia.
Basi wakati umefika wa Tanzania kama nchi nayo ipate gawio kutoka katika matumizi ya vivutio vyetu kibiashara na si kuacha watu wachache wakinufaika na huku watu wengi waliozunguka maeneo husika wakitaabika. Ethiopia imeonesha njia, tujifunze kutoka huko.Shime wataalamu wa sheria.
Sunday, February 21, 2010
Sunday, February 14, 2010
Elimu ya biashara na anguko la uchumi wa Ulimwengu
Anguko la Uchumi wa Ulimwengu limeleta madhara makubwa lakini lililowazi ni juu ya UBORA na UMAKINI kwa ujuzi unaotolewa katika shule za biashara DUNIANI.Katika Marekani swali lilikuwa juu ya majaaliwa ya elimu ya MBA (Masters of Business Administration). Katika Afrika Kusini kuna waliojiuliza kwa nini waafrika waende kusoma katika nchi ambazo zimeshindwa kuzalisha wasomi walioweza kulinda ‘msusuko’ huu.Yaani katika vyuo vya Marekani na Ulaya.
Pamoja na madai hayo bado MBA imekuwa ni elimu pendwa kwa sasa, hasa nchini Marekani kwani inakadiriwa watu wengi waliokosa kazi walirudi madarasani na wengi walirudi kusoma hizo elimu za biashara.Kampuni kubwa za kimarekani zilizoanguka zinaongozwa na wataalamu wa biashara kutoka vyuo bora kama vile Harvard, Stanford, MIT na kadhalika.
Makala haya haina nia ya kujaribu kusimulia nini kilichosababisha ‘msukosuko’ huu mkubwa wa kiuchumi duniani ulioanzia Marekani mwishoni mmwa 2007, ila tutajaribu kuangalia majaaliwa ya sekta ya Elimu ya Biashara katika Tanzania na nini tunaweza kujifunza.
Rais Barack Obama alipoingia madarakani aliendeleza mpango wa kunusuru taasisi za fedha na bima mpango ambao uliasisiwa na rais aliyemtangulia George Walker Bush Jr. Lakini mpango huu uligubikwa na utata wa matumizi yasiyorasmi ya malipo ya posho za maofisa wa ngazi za juu.
AIG (American Insurances Group), ilitumia dola milioni 165 kulipa posho ya maofisa wake. Hali hii ilifanya White House kuingilia kati na kuweka wazi kuwa haipo tayari kuona ‘bailout’ ikitumika kujilipa posho na malipo mengine manono ya maofisa wakuu wa benki na hasa katika kipindi hiki cha kupambana na anguko la Uchumi wa Ulimwengu.
Hili linaashiria kutokuwepo kwa umakini wa hali ya juu ambao unalalamikiwa na watu wengi duniani miongoni mwa watendaji wa sekta za fedha.Na hasa lililowazi ni hili la kukosekana kwa maadili, watu wachache wajilipe wakale ‘starehe’ ufukweni au kidogo kilichopo kitumike kwa ajili ya kulinda masilahi ya wengi!
Katika Marekani kuna walioenda mbali zaidi kwa kuikebehi elimu ya MBA kama ‘Masters of Disaster’. Ni wazi kuwa anguko la uchumi wa ulimwengu ni changamoto kwa elimu ya MBA na hasa shule za biashara duniani.
Kwa mwaka nchini Marekani pekee wahitimu wanaokadiriwa kufikia 100,000 uhitimu katika ’specialization’ mbalimbali za elimu ya MBA, huku asilimia 40 wakiajiriwa katika sekta ya fedha. Na sekta hii inasadikiwa ndiyo ‘chokochoko’ ya mdororo wa Uchumi ulikoanzia, pale maofisa walipokuwa wakikimbizana kutoa mikopo ili kupata ‘bonuses’ bila kujali uwezo wa mlipaji. Mikopo iliwafikia, NINJA (No Investment, No Job, No Asset) Hapo ndipo mtafutano ulipoanza, huku wakiwa na lundo kubwa la kadi wakitumia kwa mtindo wa ‘credit card’, hili lilipelekea ‘mkusanyiko’ mwingine wa madeni usiolipika kutoka sekta nyingine.
Pia kurunzi lilimulika ule utamaduni maarufu wa kuandaa mameneja, unaotambulika kama ‘Harvard Culture’. Msusuko huu wa uchumi unafanya kutimia kwa ubashiri wa Profesa Henry Mintzberg, mwanazuoni wa Masomo ya Uongozi, katika Chuo Kikuu cha McGill, Canada.
Profesa Mintzberg alipinga ‘utamaduni wa Harvard’ wa kumuandaa menejea darasani na aliweka wazi msimamo wake kuwa meneja siyo MBA, na kimsingi meneja bora anapaswa kunolewa huku akiwa anajifunza toka kwa waliomtangulia na situ kukabidhiwa wadhifa kwa msingi wa cheti.
Pamoja na yote hayo Ulimwengu umeendelea kushuhudia shule za Biashara na hasa elimu ya MBA ikipata wanafunzi wengi kuliko nafasi za udahili kama nilivyokwisha sema hapo awali. Ni wazi kuwa MBA inapendwa, na sokoni bado ipo juu.
Msususko huu wa kiuchumi umeshuhudia wasomi wa Harvard wakija na nadharia ya kuweka kiapo (oath) kwa wasomi wa MBA kuapa kukubali kulinda maadili ya biashara. Tunachojifunza hapa ni kwamba Ulimwengu wote sasa umetambua kuwa hangaiko hili la Uchumi limetokana na kukosekana kwa maadili miongoni mwa wafanyakazi wa taasisi za fedha. Hili likafanya wawe wasiri ingawa taasisi zao zilikuwa zinaanguka.Ndiyo hayo ya Ponzi Scheme!
Tanzania si kisiwa, nayo elimu ya MBA inashamiri kila kukicha vyuo vikuu vingi kwa sasa vinatoa elimu ya MBA.Huku,Mzumbe University mwaka jana ikiwa na wahitimu wanaokadiriwa kufikia 400 wakihitimu katika ‘Campus’ ya Elimu ya Biashara ya Dar-es-Salaam, pekee. Huu ni mwanzo mwema.
Lakini tunapaswa kujiuliza kama tunachokifanya darasani kuwaandaa viongozi wa biashara katika misingi ya kulinda ‘masilahi ya taifa’ au bado tunawafundisha wanafunzi ‘michakato’ ya biashara. Wanazuoni Leonidou na Kaleka wanaweka wazi kuwa elimu ya biashara kwa kiasi kikukwa imeweka msukumo katika, mbinu(strategy) mifumo na michakato badala ya ‘kufinyanga’ watu (1998)
Tanzania ya leo imekumbwa na rushwa katika sekta ya biashara huku ushindi wa rushwa kwa kupata ‘tenda’ ndiyo yamekuwa mambo ya kawaida.Sasa tunarudishiwa zaidi ya bilioni 30 za kitanzania kutokana na kashfa ya rada, Mheshimiwa Membe anaita chenji yetu!
Lakini hii ni changamoto kwa shule ya biashara, yatupasa kuandaa wasomi watakao ona kuwa kujihusisha na rushwa na kutojali masilahi ya watu wengi si jambo jema. Hapa ndipo suala la elimu ya maadili ya biashara linapoibuka.
Katika makala ya kisomi, ‘Challenges faced by business schools within newly founded catholic universities: the case of Tanzania, Mtawa (Sister) Dokta Helen A Bandiho, pia ni Mkuuwa wa Kitivo cha Biashara cha SAUT,Mwanza; anataja kuwa jukumu la shule za biashara ni kujenga jamii yenye viongozi wa biashara waliotayari kulinda masilahi ya taifa kwa kupigania masilahi ya wengi.
Akionya juu ya rushwa, ‘usiri’, matumizi mabaya ya mali ya umma,upendeleo katika zabuni havina mwisho mwema kwa shule za biashara.Hii ndiyo changamoto kubwa kwa shule za biashara kwa sasa katika Tanzania na ulimwengu kwa ujumla. Katika Tanzania ya leo huwezi kufanikiwa bila kuwa ‘network’ isiyorasmi katika biashara!
Network ya aina hii haina mwisho mwema kwani wasio na sifa ndiyo wanapata kazi na tenda, huku walio na sifa wakikata tamaa.Mara zote huwa ni majuto ambayo makala haya ikiyaorodhesha yatajaa kurasa. Mbaya zaidi wale waliotayari kuongeza bei ‘quote’ ndiyo wanaonekana kuwa wajanja, huku nchi ikiteketea. Hela zinazojenga vyumba vya madara kumi shule binafsi shule ya serikali ni vyumba viwili tu na haviishi! Hii ni hatari.
Tunahitaji kuhimarisha shule za biashara kwa kufundisha maadili ya biashara kwa kuwaandaa wanafunzi kupambana na rushwa, huku wakiwa tayari kuchukua madaraka ya kutoa maamuzi. Ingawa itaweza kutolewa hoja kuwa maadili ni suala la mtu binafsi na alivyofunzwa akiwa na familia yake.Hii ni sawa.
Lakini bado shule ya biashara ina nafasi kubwa katika kubadilisha kwa ‘kufinyanga’ wasomi wenye maadili na waliotayari kutetea masilahi ya taifa katika kila nafasi ya uongozi watakayokabidhiwa.
Kwa sasa katika Tanzania vyuo vingi vinavyotoa elimu ya biashara havina elimu ya maadili (business ethics) isipokuwa ni IFM tu waliokuwa na kozi hiyo tena kwa Shahada ya MB-International Business wanayoitoa kwa pamoja na Taasisi ya Biashara za Nje ya India.
Katika vyuo vingi kuna waliobuni Business Ethic and Law kama kozi, lakini lazima ifahamike kuwa ‘business ethics’ siyo sheria, ila ni elimu ya kumpa mwanafunzi uwezo wa kung’amua mema na mabaya, ingawa sheria inaweza ikawa inakupa nguvu.
Kwa mfano hakuna sheria itakayo kubana ukiwa unataka kufungua bar au kioski cha kitimoto karibu na msikiti. Lakini kimaadili hili si sawa. Ndivyo hivyo tunaona mifano mingi ambayo kama watoa maamuzi katika sekta ya biashara wangeweza kupata msasa kuhusu elimu ya maadili wasingaliweza kufikia maamuzi wanayoyapinga leo.
Msusuko wa Ulimwengu umefanya Harvard kufikiria kuweka kiapo kwa wasomi,wa biashara, basi yatupasa nasi kufikiria kufundisha maadili ya biashara, kwani mashaka yetu ya ubadhirifu wa mali ya umma, rushwa, upendeleo na mengine ya hovyo yanachangiwa na kukosa maadili.
MUNGU IBARIKI TANZANIA,
MUNGU IBARIKI AFRIKA.
Pamoja na madai hayo bado MBA imekuwa ni elimu pendwa kwa sasa, hasa nchini Marekani kwani inakadiriwa watu wengi waliokosa kazi walirudi madarasani na wengi walirudi kusoma hizo elimu za biashara.Kampuni kubwa za kimarekani zilizoanguka zinaongozwa na wataalamu wa biashara kutoka vyuo bora kama vile Harvard, Stanford, MIT na kadhalika.
Makala haya haina nia ya kujaribu kusimulia nini kilichosababisha ‘msukosuko’ huu mkubwa wa kiuchumi duniani ulioanzia Marekani mwishoni mmwa 2007, ila tutajaribu kuangalia majaaliwa ya sekta ya Elimu ya Biashara katika Tanzania na nini tunaweza kujifunza.
Rais Barack Obama alipoingia madarakani aliendeleza mpango wa kunusuru taasisi za fedha na bima mpango ambao uliasisiwa na rais aliyemtangulia George Walker Bush Jr. Lakini mpango huu uligubikwa na utata wa matumizi yasiyorasmi ya malipo ya posho za maofisa wa ngazi za juu.
AIG (American Insurances Group), ilitumia dola milioni 165 kulipa posho ya maofisa wake. Hali hii ilifanya White House kuingilia kati na kuweka wazi kuwa haipo tayari kuona ‘bailout’ ikitumika kujilipa posho na malipo mengine manono ya maofisa wakuu wa benki na hasa katika kipindi hiki cha kupambana na anguko la Uchumi wa Ulimwengu.
Hili linaashiria kutokuwepo kwa umakini wa hali ya juu ambao unalalamikiwa na watu wengi duniani miongoni mwa watendaji wa sekta za fedha.Na hasa lililowazi ni hili la kukosekana kwa maadili, watu wachache wajilipe wakale ‘starehe’ ufukweni au kidogo kilichopo kitumike kwa ajili ya kulinda masilahi ya wengi!
Katika Marekani kuna walioenda mbali zaidi kwa kuikebehi elimu ya MBA kama ‘Masters of Disaster’. Ni wazi kuwa anguko la uchumi wa ulimwengu ni changamoto kwa elimu ya MBA na hasa shule za biashara duniani.
Kwa mwaka nchini Marekani pekee wahitimu wanaokadiriwa kufikia 100,000 uhitimu katika ’specialization’ mbalimbali za elimu ya MBA, huku asilimia 40 wakiajiriwa katika sekta ya fedha. Na sekta hii inasadikiwa ndiyo ‘chokochoko’ ya mdororo wa Uchumi ulikoanzia, pale maofisa walipokuwa wakikimbizana kutoa mikopo ili kupata ‘bonuses’ bila kujali uwezo wa mlipaji. Mikopo iliwafikia, NINJA (No Investment, No Job, No Asset) Hapo ndipo mtafutano ulipoanza, huku wakiwa na lundo kubwa la kadi wakitumia kwa mtindo wa ‘credit card’, hili lilipelekea ‘mkusanyiko’ mwingine wa madeni usiolipika kutoka sekta nyingine.
Pia kurunzi lilimulika ule utamaduni maarufu wa kuandaa mameneja, unaotambulika kama ‘Harvard Culture’. Msusuko huu wa uchumi unafanya kutimia kwa ubashiri wa Profesa Henry Mintzberg, mwanazuoni wa Masomo ya Uongozi, katika Chuo Kikuu cha McGill, Canada.
Profesa Mintzberg alipinga ‘utamaduni wa Harvard’ wa kumuandaa menejea darasani na aliweka wazi msimamo wake kuwa meneja siyo MBA, na kimsingi meneja bora anapaswa kunolewa huku akiwa anajifunza toka kwa waliomtangulia na situ kukabidhiwa wadhifa kwa msingi wa cheti.
Pamoja na yote hayo Ulimwengu umeendelea kushuhudia shule za Biashara na hasa elimu ya MBA ikipata wanafunzi wengi kuliko nafasi za udahili kama nilivyokwisha sema hapo awali. Ni wazi kuwa MBA inapendwa, na sokoni bado ipo juu.
Msususko huu wa kiuchumi umeshuhudia wasomi wa Harvard wakija na nadharia ya kuweka kiapo (oath) kwa wasomi wa MBA kuapa kukubali kulinda maadili ya biashara. Tunachojifunza hapa ni kwamba Ulimwengu wote sasa umetambua kuwa hangaiko hili la Uchumi limetokana na kukosekana kwa maadili miongoni mwa wafanyakazi wa taasisi za fedha. Hili likafanya wawe wasiri ingawa taasisi zao zilikuwa zinaanguka.Ndiyo hayo ya Ponzi Scheme!
Tanzania si kisiwa, nayo elimu ya MBA inashamiri kila kukicha vyuo vikuu vingi kwa sasa vinatoa elimu ya MBA.Huku,Mzumbe University mwaka jana ikiwa na wahitimu wanaokadiriwa kufikia 400 wakihitimu katika ‘Campus’ ya Elimu ya Biashara ya Dar-es-Salaam, pekee. Huu ni mwanzo mwema.
Lakini tunapaswa kujiuliza kama tunachokifanya darasani kuwaandaa viongozi wa biashara katika misingi ya kulinda ‘masilahi ya taifa’ au bado tunawafundisha wanafunzi ‘michakato’ ya biashara. Wanazuoni Leonidou na Kaleka wanaweka wazi kuwa elimu ya biashara kwa kiasi kikukwa imeweka msukumo katika, mbinu(strategy) mifumo na michakato badala ya ‘kufinyanga’ watu (1998)
Tanzania ya leo imekumbwa na rushwa katika sekta ya biashara huku ushindi wa rushwa kwa kupata ‘tenda’ ndiyo yamekuwa mambo ya kawaida.Sasa tunarudishiwa zaidi ya bilioni 30 za kitanzania kutokana na kashfa ya rada, Mheshimiwa Membe anaita chenji yetu!
Lakini hii ni changamoto kwa shule ya biashara, yatupasa kuandaa wasomi watakao ona kuwa kujihusisha na rushwa na kutojali masilahi ya watu wengi si jambo jema. Hapa ndipo suala la elimu ya maadili ya biashara linapoibuka.
Katika makala ya kisomi, ‘Challenges faced by business schools within newly founded catholic universities: the case of Tanzania, Mtawa (Sister) Dokta Helen A Bandiho, pia ni Mkuuwa wa Kitivo cha Biashara cha SAUT,Mwanza; anataja kuwa jukumu la shule za biashara ni kujenga jamii yenye viongozi wa biashara waliotayari kulinda masilahi ya taifa kwa kupigania masilahi ya wengi.
Akionya juu ya rushwa, ‘usiri’, matumizi mabaya ya mali ya umma,upendeleo katika zabuni havina mwisho mwema kwa shule za biashara.Hii ndiyo changamoto kubwa kwa shule za biashara kwa sasa katika Tanzania na ulimwengu kwa ujumla. Katika Tanzania ya leo huwezi kufanikiwa bila kuwa ‘network’ isiyorasmi katika biashara!
Network ya aina hii haina mwisho mwema kwani wasio na sifa ndiyo wanapata kazi na tenda, huku walio na sifa wakikata tamaa.Mara zote huwa ni majuto ambayo makala haya ikiyaorodhesha yatajaa kurasa. Mbaya zaidi wale waliotayari kuongeza bei ‘quote’ ndiyo wanaonekana kuwa wajanja, huku nchi ikiteketea. Hela zinazojenga vyumba vya madara kumi shule binafsi shule ya serikali ni vyumba viwili tu na haviishi! Hii ni hatari.
Tunahitaji kuhimarisha shule za biashara kwa kufundisha maadili ya biashara kwa kuwaandaa wanafunzi kupambana na rushwa, huku wakiwa tayari kuchukua madaraka ya kutoa maamuzi. Ingawa itaweza kutolewa hoja kuwa maadili ni suala la mtu binafsi na alivyofunzwa akiwa na familia yake.Hii ni sawa.
Lakini bado shule ya biashara ina nafasi kubwa katika kubadilisha kwa ‘kufinyanga’ wasomi wenye maadili na waliotayari kutetea masilahi ya taifa katika kila nafasi ya uongozi watakayokabidhiwa.
Kwa sasa katika Tanzania vyuo vingi vinavyotoa elimu ya biashara havina elimu ya maadili (business ethics) isipokuwa ni IFM tu waliokuwa na kozi hiyo tena kwa Shahada ya MB-International Business wanayoitoa kwa pamoja na Taasisi ya Biashara za Nje ya India.
Katika vyuo vingi kuna waliobuni Business Ethic and Law kama kozi, lakini lazima ifahamike kuwa ‘business ethics’ siyo sheria, ila ni elimu ya kumpa mwanafunzi uwezo wa kung’amua mema na mabaya, ingawa sheria inaweza ikawa inakupa nguvu.
Kwa mfano hakuna sheria itakayo kubana ukiwa unataka kufungua bar au kioski cha kitimoto karibu na msikiti. Lakini kimaadili hili si sawa. Ndivyo hivyo tunaona mifano mingi ambayo kama watoa maamuzi katika sekta ya biashara wangeweza kupata msasa kuhusu elimu ya maadili wasingaliweza kufikia maamuzi wanayoyapinga leo.
Msusuko wa Ulimwengu umefanya Harvard kufikiria kuweka kiapo kwa wasomi,wa biashara, basi yatupasa nasi kufikiria kufundisha maadili ya biashara, kwani mashaka yetu ya ubadhirifu wa mali ya umma, rushwa, upendeleo na mengine ya hovyo yanachangiwa na kukosa maadili.
MUNGU IBARIKI TANZANIA,
MUNGU IBARIKI AFRIKA.
Sunday, February 7, 2010
Tunachojifunza kutokana kupanda kwa bei ya mchele duniani
Mchele unaozalishwa kwa asilimia 90 katika bara la Asia, ni asilimia saba tu huingia katika biashara ya Ulimwengu. Ulimwengu bado unakumbuka hofu ya kitisho cha chakula ilivyopandisha bidhaa hii, huku ikifanya baadhi ya nchi kama Philippines kukosa shehena aliyoihitaji pamoja na dau kubwa la dola 680 kwa tani wauzaji na ‘waroho’ wa pesa walikataa kuiuzia tani 500,000 alizohitaji.
Tangu Januari 2008 biashara ya Ulimwengu ya chakula imekumbwa na msusuko wa kupanda kwa bei, huku mchele ambao ni chakula cha watu wengi walio masikini katika Asia ukipanda maradufu.Hali iliyofanya kuleta hofu zaidi miongoini mwa wa jamii ya kimataifa.
Kwa sasa bei ya mchele inaonekana kushuka kwa mujibu wa takwimu za FAO. Lakini Idara ya chakula ya Marekani inaonya kuwa hali bado ni ‘tete’ hasa kwa mchele na bei yake kutengemaa katika siku za karibuni.
Tanzania si muagizaji mkubwa wa mchele katika Afrika, lakini umuhimu wa zao la mchele kutoka Asia hakuna asiyeujua katika nchi hii. Mchele umekuwa siyo chakula kikuu hivyo kufanya mara zote iwe ni kimbilio letu wakati wa njaa.Mchele kutoka Thailand na Vietnam huwa ndiyo chakula mkombozi wetu wakati wa njaa.Kuna aina maarufu kama kitumbo na V.I.P ni aina ya Indica, wenye thamani ndogo katika soko la dunia.
Bei ya mchele ya ulimwengu inaonakana kuwa tata, kwa vile kuna madai kuwa India imeanza kupita kupita kwa nchi wazalishaji huku ikitangaza kuhitaji shehena ya mchele. Hii ni dalili ya wazi kuwa kitisho hiki cha India kuna jambo laja.
Ripoti ya FAO, Food Outlook, 2009, inabainisha wazi kuwa, India ipo sokoni ikiwa inavizia maeneo ya kununua mchele. Nia ikiwa kuongeza shehena yake ya mchele kwa tani milioni 9 zaidi. Ingawa haikuwa na uhakika juu ya madai ya kupipita kwa India katika kutafuta wauzaji wa mchele.Biashara ya Ulimwengu ya mchele inakadiriwa kupanda kwa tani 800,000 zaidi ya mwaka jana.
Wadadisi wa biashara ya mchele duniani wanabashiri wazi kuwa mahitaji ya ulaji ya mchele yanakadiriwa kupungua katika Asia.Lakini wanaonya kuwa kupungua kwa ulaji kwa jamii za Uchina, Thailand, India, Korea na Japan haimaanishi kuwa mchele utapungua bei kwa vile umekosa walaji.
Ila kitakachotokea ni kwamba uzalishaji wa mchele utapungua, kutokana na ukweli kuwa mashamba mengi yananyakuliwa kwa ajili ya ujenzi wa makazi kutokana na ukuaji wa miji mingi katika Asia.
Ukuaji wa miji unakadiriwa pia kuchochea ujenzi wa viwanda na barabara hali ambayo shirika la Utafiti wa mchele (IRI) lenye makazi yake Phillipines; linaelezea kuwa itapunguza ardhi kwa kilimo cha mpunga.
Pia kuna taarifa kuwa kuimarika kwa kipato cha familia kutapunguza walaji wa mchele, hali inayokadiriwa kuchangiwa mno na mafanikio ya uzazi wa mpango katika nchi nyingi za Asia ya Kusini na hasa Uchina.
Ukuaji huu wa chumo la familia unapelekea familia nyingi kubadili iana ya chakula, basi hili linajionesha wazi na kurufurika kwa maduka ya makubwa ‘supermarkets’ kutoka magharibi katika nchi hizi. Maduka kama Tesco, Asda, Mark Spencer Spencer na WalMart, wauzaji wa ‘fast food’ McDonalds, Kentucky Fried Chicken, StarBuck na kadhalika. Jamii ya Asia ya leo si walaji mchele tena, bali hupenda kula zaidi vyakula vya 'magharibi’
Mabadiliko ya chakula yanapeleka mbinyo tena katika ardhi iliyokuwa inatumika kulima mchele, sasa hutumika kulima mboga mboga , matunda, kukidhi mahitaji na mabadiliko ya jamii za Asia.
Mwenendo huu wa matumizi ya mchele katika Asia yanatufanya tujiulize juu ya siku za baadaye kwa Afrika ambayo hutumia Asia kama kapu lake la chakula wakati wa njaa?
Katika Afrika waagizaji wakubwa wa mchele ni Nigeria ambayo huagiza asilimia 6 na Senegal asilimia 4 ya mchele unaoingia katika soko la Ulimwengu, huku maeneo mengi yakiwa si walaji wakubwa wa mchele hadi ukame au kitisho cha njaa ndipo hukimbilia katika masoko ya Asia.
Tanzania ni miongoni mwa nchi ambazo si walaji wakubwa wa mchele, chakula kikuu ni mahindi. Pamoja na hayo lakini lililowazi ni kwamba mchele kutoka Asia ni mkombozi wa njaa katika Tanzania.
Indica, ni aina ya mchele ambao ni wenye kiwango cha chini cha ubora ukiwa umevunjika kwa asimilia 25, mara nyingi ulikuwa umeonekana kukosa soko lakini hali ya mambo hadi mwanzoni mwa Januari mwaka huu, ilionesha kuwa mchele huu utapata wateja, hii ni baada ya Philippines kuinngia sokoni akiwa ananunua aina hii ya mchele.
Lakini lililowazi ni kwamba hali ya bei ya biashara ya mchele inatarajiwa kupanda Ulimwenguni. Asia ikiwa mlimaji mkubwa wa mpunga, ndiyo pia kuna walaji wakubwa, lakini nchi nyingi za eneo hilo zimeweka vikwazo kwa biashara ya mchele kwa kuweka kodi ya mauzo ya nje na hata kuzuia kwa hofu ya kutokea upungufu wa chakula na kuathiri raia wengi walio maskini.
Tunachoweza kujifunza kwa mwenendo wa biashara ya mchele, Afrika inahitaji kuongeza nguvu katika kilimo cha chakula. Tangu azimio la Maputo kupitishwa kwa nchi za Afrika kuweka bajeti ya asilimia kumi katika kilimo ni nchi chache zimeweza kufikia lengo hili.
Hali ya mambo katika Asia, ambako mchele unalimwa inaonekana kubadilika mno, hasa kutokana na ukweli kuwa ‘style’ ya ulaji imebadilika na kufanya jamii nyingi za huko kupenda kula vyakula vya magharibi,hiki ni kitisho kwa Afrika.
Ingawa mabadiliko haya kasi yake kitakwimu hazipo wazi, lakini ongezo la maduka makubwa ya magharibi na kuongezeka uzito kunakosabishwa na ulaji wa ‘junk food’ ni dalili kuwa sasa Asia inaondoka katika kula mchele kama chakula kikuu.
Afrika haina budi kujipanga, katika kuhakikisha inalisha jamii ya watu wake, kwani kwa sasa hali ya uhakika wa chakula na biashara ya chakula duniani imebadilika mno.
Tuchague moja, kulima mau na viepepeo au kulima mazao ya chakula. Jibu tunalo waafrika wenyewe. Profesa Steve Carter na Dr Kiefer Lee, wanaonya juu ya hatari ya kufikiria zaidi soko la nje na kujitahidi kukidhi mahitaji ya soko hilo, katika kitabu Global Marketing Management wanaandika ‘biashara hii itakuwa haina maana kama chumo lake na zaidi litakwenda tena katika kuagiza kitu ambacho nchi inahitaji zaidi’
Ni wazi kuwa Afrika inahitaji zaidi chakula kuliko chumo hilo la vipepeo au maua, ambayo hata soko la ndani hakuna anayevitumia. Kenya sasa inahaha kuhamasisha matumizi ya maua kwa soko la ndani; kwani asilimia 96, hutegemea soko la nje. Ni wazi kuwa ‘ndoto’ hizi haziwezi kutimia, kwani maua si hitaji la wakenya.
Vinyo hivyo kwa nchi nyingine za Afrika ya joto tumejikuta tunaingia katika mtego kama huu, wa kuhangaika kufikia matarajio ya soko la Ulaya wakati, faida ya huko kimsingi baada ya muda inarudi tena na ziada inahitajika katika kununua chakula.
Hatumaanishi kuwa hii biashara ni mbaya, lakini yatupasa kulinganisha na kutambua mahitaji yetu je yametimizwa? Basi tuweke nguvu katika kilimo cha mazao ya chakula na tuache ‘ushabiki’, kwani hakuna mgeni atakaye kuja Afrika kuja kulima mpunga.
Tangu Januari 2008 biashara ya Ulimwengu ya chakula imekumbwa na msusuko wa kupanda kwa bei, huku mchele ambao ni chakula cha watu wengi walio masikini katika Asia ukipanda maradufu.Hali iliyofanya kuleta hofu zaidi miongoini mwa wa jamii ya kimataifa.
Kwa sasa bei ya mchele inaonekana kushuka kwa mujibu wa takwimu za FAO. Lakini Idara ya chakula ya Marekani inaonya kuwa hali bado ni ‘tete’ hasa kwa mchele na bei yake kutengemaa katika siku za karibuni.
Tanzania si muagizaji mkubwa wa mchele katika Afrika, lakini umuhimu wa zao la mchele kutoka Asia hakuna asiyeujua katika nchi hii. Mchele umekuwa siyo chakula kikuu hivyo kufanya mara zote iwe ni kimbilio letu wakati wa njaa.Mchele kutoka Thailand na Vietnam huwa ndiyo chakula mkombozi wetu wakati wa njaa.Kuna aina maarufu kama kitumbo na V.I.P ni aina ya Indica, wenye thamani ndogo katika soko la dunia.
Bei ya mchele ya ulimwengu inaonakana kuwa tata, kwa vile kuna madai kuwa India imeanza kupita kupita kwa nchi wazalishaji huku ikitangaza kuhitaji shehena ya mchele. Hii ni dalili ya wazi kuwa kitisho hiki cha India kuna jambo laja.
Ripoti ya FAO, Food Outlook, 2009, inabainisha wazi kuwa, India ipo sokoni ikiwa inavizia maeneo ya kununua mchele. Nia ikiwa kuongeza shehena yake ya mchele kwa tani milioni 9 zaidi. Ingawa haikuwa na uhakika juu ya madai ya kupipita kwa India katika kutafuta wauzaji wa mchele.Biashara ya Ulimwengu ya mchele inakadiriwa kupanda kwa tani 800,000 zaidi ya mwaka jana.
Wadadisi wa biashara ya mchele duniani wanabashiri wazi kuwa mahitaji ya ulaji ya mchele yanakadiriwa kupungua katika Asia.Lakini wanaonya kuwa kupungua kwa ulaji kwa jamii za Uchina, Thailand, India, Korea na Japan haimaanishi kuwa mchele utapungua bei kwa vile umekosa walaji.
Ila kitakachotokea ni kwamba uzalishaji wa mchele utapungua, kutokana na ukweli kuwa mashamba mengi yananyakuliwa kwa ajili ya ujenzi wa makazi kutokana na ukuaji wa miji mingi katika Asia.
Ukuaji wa miji unakadiriwa pia kuchochea ujenzi wa viwanda na barabara hali ambayo shirika la Utafiti wa mchele (IRI) lenye makazi yake Phillipines; linaelezea kuwa itapunguza ardhi kwa kilimo cha mpunga.
Pia kuna taarifa kuwa kuimarika kwa kipato cha familia kutapunguza walaji wa mchele, hali inayokadiriwa kuchangiwa mno na mafanikio ya uzazi wa mpango katika nchi nyingi za Asia ya Kusini na hasa Uchina.
Ukuaji huu wa chumo la familia unapelekea familia nyingi kubadili iana ya chakula, basi hili linajionesha wazi na kurufurika kwa maduka ya makubwa ‘supermarkets’ kutoka magharibi katika nchi hizi. Maduka kama Tesco, Asda, Mark Spencer Spencer na WalMart, wauzaji wa ‘fast food’ McDonalds, Kentucky Fried Chicken, StarBuck na kadhalika. Jamii ya Asia ya leo si walaji mchele tena, bali hupenda kula zaidi vyakula vya 'magharibi’
Mabadiliko ya chakula yanapeleka mbinyo tena katika ardhi iliyokuwa inatumika kulima mchele, sasa hutumika kulima mboga mboga , matunda, kukidhi mahitaji na mabadiliko ya jamii za Asia.
Mwenendo huu wa matumizi ya mchele katika Asia yanatufanya tujiulize juu ya siku za baadaye kwa Afrika ambayo hutumia Asia kama kapu lake la chakula wakati wa njaa?
Katika Afrika waagizaji wakubwa wa mchele ni Nigeria ambayo huagiza asilimia 6 na Senegal asilimia 4 ya mchele unaoingia katika soko la Ulimwengu, huku maeneo mengi yakiwa si walaji wakubwa wa mchele hadi ukame au kitisho cha njaa ndipo hukimbilia katika masoko ya Asia.
Tanzania ni miongoni mwa nchi ambazo si walaji wakubwa wa mchele, chakula kikuu ni mahindi. Pamoja na hayo lakini lililowazi ni kwamba mchele kutoka Asia ni mkombozi wa njaa katika Tanzania.
Indica, ni aina ya mchele ambao ni wenye kiwango cha chini cha ubora ukiwa umevunjika kwa asimilia 25, mara nyingi ulikuwa umeonekana kukosa soko lakini hali ya mambo hadi mwanzoni mwa Januari mwaka huu, ilionesha kuwa mchele huu utapata wateja, hii ni baada ya Philippines kuinngia sokoni akiwa ananunua aina hii ya mchele.
Lakini lililowazi ni kwamba hali ya bei ya biashara ya mchele inatarajiwa kupanda Ulimwenguni. Asia ikiwa mlimaji mkubwa wa mpunga, ndiyo pia kuna walaji wakubwa, lakini nchi nyingi za eneo hilo zimeweka vikwazo kwa biashara ya mchele kwa kuweka kodi ya mauzo ya nje na hata kuzuia kwa hofu ya kutokea upungufu wa chakula na kuathiri raia wengi walio maskini.
Tunachoweza kujifunza kwa mwenendo wa biashara ya mchele, Afrika inahitaji kuongeza nguvu katika kilimo cha chakula. Tangu azimio la Maputo kupitishwa kwa nchi za Afrika kuweka bajeti ya asilimia kumi katika kilimo ni nchi chache zimeweza kufikia lengo hili.
Hali ya mambo katika Asia, ambako mchele unalimwa inaonekana kubadilika mno, hasa kutokana na ukweli kuwa ‘style’ ya ulaji imebadilika na kufanya jamii nyingi za huko kupenda kula vyakula vya magharibi,hiki ni kitisho kwa Afrika.
Ingawa mabadiliko haya kasi yake kitakwimu hazipo wazi, lakini ongezo la maduka makubwa ya magharibi na kuongezeka uzito kunakosabishwa na ulaji wa ‘junk food’ ni dalili kuwa sasa Asia inaondoka katika kula mchele kama chakula kikuu.
Afrika haina budi kujipanga, katika kuhakikisha inalisha jamii ya watu wake, kwani kwa sasa hali ya uhakika wa chakula na biashara ya chakula duniani imebadilika mno.
Tuchague moja, kulima mau na viepepeo au kulima mazao ya chakula. Jibu tunalo waafrika wenyewe. Profesa Steve Carter na Dr Kiefer Lee, wanaonya juu ya hatari ya kufikiria zaidi soko la nje na kujitahidi kukidhi mahitaji ya soko hilo, katika kitabu Global Marketing Management wanaandika ‘biashara hii itakuwa haina maana kama chumo lake na zaidi litakwenda tena katika kuagiza kitu ambacho nchi inahitaji zaidi’
Ni wazi kuwa Afrika inahitaji zaidi chakula kuliko chumo hilo la vipepeo au maua, ambayo hata soko la ndani hakuna anayevitumia. Kenya sasa inahaha kuhamasisha matumizi ya maua kwa soko la ndani; kwani asilimia 96, hutegemea soko la nje. Ni wazi kuwa ‘ndoto’ hizi haziwezi kutimia, kwani maua si hitaji la wakenya.
Vinyo hivyo kwa nchi nyingine za Afrika ya joto tumejikuta tunaingia katika mtego kama huu, wa kuhangaika kufikia matarajio ya soko la Ulaya wakati, faida ya huko kimsingi baada ya muda inarudi tena na ziada inahitajika katika kununua chakula.
Hatumaanishi kuwa hii biashara ni mbaya, lakini yatupasa kulinganisha na kutambua mahitaji yetu je yametimizwa? Basi tuweke nguvu katika kilimo cha mazao ya chakula na tuache ‘ushabiki’, kwani hakuna mgeni atakaye kuja Afrika kuja kulima mpunga.
Monday, January 18, 2010
Ni muda muafaka kuongeza umri wa kustaafu
Majuma machache yaliyopita vyombo vya habari vya Tanzania. vilipambwa na sakata la serikali kumnyima ajira ya mkataba, mwanazuoni nguli wa siasa za kimataifa Profesa Mwesiga Baregu wa Chuo Kikuu cha Dar-Es-Salaam (UDSM).
Waziri mwenye dhamana, Mheshimiwa Hawa Abdulreihman Ghasia, aliweka wazi kuwa serikali kwa sasa haina nia ya kumpa mkataba mpya Profesa Baregu, baada ya kumpatia mara tatu tangu alipostaafu mwaka 1999, akiwa na miaka 55.
Tangu suala la kunyimwa mkataba kwa nguli huyu lilipoibuliwa katika vyombo vya habari, kuna makundi mawili makubwa yameibuka katika kuangalia, uhalali wa kama Profesa ameonewa au serikali ipo sahihi kusitisha kumpa mkataba.
Kuna waliojikita katika itikadi za kisiasa, ingawa waziri pia amegusia hilo kuwa ndiyo kiini cha kusitisha mkataba mpya kwa gwiji huyu. Lakini kuna madai kuwa wapo wana CCM mbona wamepata, wakienda mbali zaidi wakihusisha ukosoaji wake kwa serikali kuwa ndiyo kigingi cha yeye kutemwa UDSM.
Kichuguu cha pili kilikuwa na wale wanaoona kuwa maamuzi haya ni sahihi ingawa hawa hawakupata nafasi ya kuhojiwa sana na vyombo vya habari, huku wakiweka wazi kuwa sasa huu ni wakati wa damu changa kuchukua nafasi katika taasisi mbalimbali za serikali.
Makala haya haina nia ya kusema kati ya hivyo vichuguu viwili na hoja zao kipi kipo sahihi au yupi amekosea, la hasha ila itajaribu kupitia umuhimmu wa kuangalia nini tunajifunza kama 'nchi' kuhusu sakata hili, la Profesa Baregu.Serikali imekwisha hitimisha.
Somo tunalotaka kulijadili katika makala haya ni kuhusu umri wa kustaafu katika Tanzania.Na hasa kwa wanazuoni au wataalamu wengine ambao serikali hutumia gharama kubwa kuwasomesha.
Naweka wazi msimamo wangu kuwa umri wa kustaafu unapaswa kuongezwa na hasa katika kada za walimu wa vyuo vikuu. Kwa sasa kuna wanaostaafu katika 55 na wengine 60 kwa manufaa ya umma.
Ulimwengu wa leo watu wengi wananafasi kubwa yakuishi maisha marefu hii ni kutokana na mafanikio ya kisayansi ambayo yameweza kuboresha viwango vya ubora wa maisha kwa wale wanaozingatia na kufuatilia kwa ukaribu. Magonjwa ambayo yalikuwa tishio si tena tishio kwa binadamu.
Pia mafanikio ya kisayansi yanampa nafasi binadamu kuweza kufanya kazi kwa muda mrefu, wakati zamani miaka 55, ni umri uliokuwa kweli umechoka kweli kweli. Mfano Mzuri ni huyo Profesa, tangu astaafu amepewa mikataba mitatu na bado yu mwenye siha nzuri na anaonekana anaweza kumudu mikiki mikiki ya kazi yake.
Katika Tanzania, kustaafu katika miaka chini ya 65 ni pigo kwa nchi na hasa wahadhiri ambao wengi leo hii tulionao wako mbioni kustaafu, vyuo vingi vinakabiliwa na hatari ya kukosa hawa magwiji katika miaka mitano ijayo.
Inakadiriwa katika miaka mitano ijayo wengi ya wanataaluma waliobobea katika shahada za uzamivu watakuwa wamestaafu wakiwa na umri wa miaka 60. Kimsingi hii ni hasara kwa nchi.
Hasara kwa sababu, wengi ya wanazuoni tulionao wamapata PhD wakiwa na zaidi ya miaka 45 hadi 50. Sasa ukiangalia gharama za kumsomesha mwanafunzi wa PhD alafu anatumika chini ya miaka 10 anastaafu ni nchi ndiyo inapata hasara.
Hili suala la kuomba kuongeza muda wa kustaafu walau ufikie miaka 65 si jambo geni, na wala siyo hoja mpya katika Tanzania.Kati ya watu wanaopigia chapuo kuongezwa kwa umri wa kustaafu ni Balozi Juma Mwapachu, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Sisi tumechelewa kusoma, na mifumo yetu mara nyingi inatubana kupata wanazuoni walio na umri chini ya miaka 30 wakiwa na PhD. labda katika miaka 10 ijayo tutakuwa na watanzania walio na PhD wakiwa chini ya 30 hii baada ya serikali ya awamu ya tatu kuhimiza kupeleka watoto shule mapema.
Na ujio wa shule binafsi umefungua mwanya kwa vijana wa kitanzania kwenda shule wakiwa na wastani wa miaka 4 hadi 6 kuanza darasa la kwanza huku wakirushwa baadhi ya madarasa, hasa la saba na wangine wakitumia elimu ya nje kama Kenya na Uganda kusonga mbele katika vyuo vikuu vya huko.
Ila kwa wale tuliosoma Tanzania ni wazi kuwa kupata PhD si chini ya miaka 45, na kupata Uprofesa kama ngazi ya juu ya kielimu katika kufundisha inaweza kuchukua zaidi ya miaka 10 kwa Tanzania.Ukijumlisha na uchelevu wa kwenda shule huko nyuma wengi wanakuwa maprofesa bado miaka michache kustaafu. Hawa ndiyo magwiji walioiva.
Sasa kwa nini wameiva sasa, ndiyo tunawapa taarifa ya kusataafu!Hapa pana ulakini.Katika nchi za magharibi kustaafu ni miaka 65, na wengi huku wamepata PhD wakiwa chini ya miaka 25. Hivyo anaitumikia nchi yake kwa zaidi ya 30.
Ni wazi kuwa atarudisha fedha ya walipa kodi kwa kazi atakayoifanyia nchi yake.
Hasara yake ni kwamba wakati tumetumia pesa nyingi kuwasomesha katika vyuo vya nchi za magharibi kwa gharama zisizopungua milioni 100 kwa mtu mmoja kwa PhD tunamtumia chini ya miaka 10,kwa vile tu sheria inasema astaafu chini ya miaka 65!
Pesa nyingine zinakuja kama mikopo, hivyo hata mkopo haujalipwa na mtu hajaitumikia jamii yake anaambimwa astaafu kwa manufaa ya umma.
Ni sheria inapaswa kufuatwa. Lakini sheria hii kwa mmtazamo wangu nahisi ina matatizo na hasa kwa nchi yetu hii changa. Mbona Uingereza wanastaafu wakiwa na miaka 65.
Lengo kuu la sheria au taratibu za jamii yoyote ni kuwatumia jamii husika, sasa sheria hii inaonekana haina manufaa kwetu yatupasa kuijadili na kutafuta suluhu ya kudumu.
Rai yetu ni kwamba huu ni wakati muafaka wa kufikiria kuongeza kwa umri wa kustaafu iwe kwa hiyari au kwa manufaa ya umma umri uwe miaka 65.
Waziri mwenye dhamana, Mheshimiwa Hawa Abdulreihman Ghasia, aliweka wazi kuwa serikali kwa sasa haina nia ya kumpa mkataba mpya Profesa Baregu, baada ya kumpatia mara tatu tangu alipostaafu mwaka 1999, akiwa na miaka 55.
Tangu suala la kunyimwa mkataba kwa nguli huyu lilipoibuliwa katika vyombo vya habari, kuna makundi mawili makubwa yameibuka katika kuangalia, uhalali wa kama Profesa ameonewa au serikali ipo sahihi kusitisha kumpa mkataba.
Kuna waliojikita katika itikadi za kisiasa, ingawa waziri pia amegusia hilo kuwa ndiyo kiini cha kusitisha mkataba mpya kwa gwiji huyu. Lakini kuna madai kuwa wapo wana CCM mbona wamepata, wakienda mbali zaidi wakihusisha ukosoaji wake kwa serikali kuwa ndiyo kigingi cha yeye kutemwa UDSM.
Kichuguu cha pili kilikuwa na wale wanaoona kuwa maamuzi haya ni sahihi ingawa hawa hawakupata nafasi ya kuhojiwa sana na vyombo vya habari, huku wakiweka wazi kuwa sasa huu ni wakati wa damu changa kuchukua nafasi katika taasisi mbalimbali za serikali.
Makala haya haina nia ya kusema kati ya hivyo vichuguu viwili na hoja zao kipi kipo sahihi au yupi amekosea, la hasha ila itajaribu kupitia umuhimmu wa kuangalia nini tunajifunza kama 'nchi' kuhusu sakata hili, la Profesa Baregu.Serikali imekwisha hitimisha.
Somo tunalotaka kulijadili katika makala haya ni kuhusu umri wa kustaafu katika Tanzania.Na hasa kwa wanazuoni au wataalamu wengine ambao serikali hutumia gharama kubwa kuwasomesha.
Naweka wazi msimamo wangu kuwa umri wa kustaafu unapaswa kuongezwa na hasa katika kada za walimu wa vyuo vikuu. Kwa sasa kuna wanaostaafu katika 55 na wengine 60 kwa manufaa ya umma.
Ulimwengu wa leo watu wengi wananafasi kubwa yakuishi maisha marefu hii ni kutokana na mafanikio ya kisayansi ambayo yameweza kuboresha viwango vya ubora wa maisha kwa wale wanaozingatia na kufuatilia kwa ukaribu. Magonjwa ambayo yalikuwa tishio si tena tishio kwa binadamu.
Pia mafanikio ya kisayansi yanampa nafasi binadamu kuweza kufanya kazi kwa muda mrefu, wakati zamani miaka 55, ni umri uliokuwa kweli umechoka kweli kweli. Mfano Mzuri ni huyo Profesa, tangu astaafu amepewa mikataba mitatu na bado yu mwenye siha nzuri na anaonekana anaweza kumudu mikiki mikiki ya kazi yake.
Katika Tanzania, kustaafu katika miaka chini ya 65 ni pigo kwa nchi na hasa wahadhiri ambao wengi leo hii tulionao wako mbioni kustaafu, vyuo vingi vinakabiliwa na hatari ya kukosa hawa magwiji katika miaka mitano ijayo.
Inakadiriwa katika miaka mitano ijayo wengi ya wanataaluma waliobobea katika shahada za uzamivu watakuwa wamestaafu wakiwa na umri wa miaka 60. Kimsingi hii ni hasara kwa nchi.
Hasara kwa sababu, wengi ya wanazuoni tulionao wamapata PhD wakiwa na zaidi ya miaka 45 hadi 50. Sasa ukiangalia gharama za kumsomesha mwanafunzi wa PhD alafu anatumika chini ya miaka 10 anastaafu ni nchi ndiyo inapata hasara.
Hili suala la kuomba kuongeza muda wa kustaafu walau ufikie miaka 65 si jambo geni, na wala siyo hoja mpya katika Tanzania.Kati ya watu wanaopigia chapuo kuongezwa kwa umri wa kustaafu ni Balozi Juma Mwapachu, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Sisi tumechelewa kusoma, na mifumo yetu mara nyingi inatubana kupata wanazuoni walio na umri chini ya miaka 30 wakiwa na PhD. labda katika miaka 10 ijayo tutakuwa na watanzania walio na PhD wakiwa chini ya 30 hii baada ya serikali ya awamu ya tatu kuhimiza kupeleka watoto shule mapema.
Na ujio wa shule binafsi umefungua mwanya kwa vijana wa kitanzania kwenda shule wakiwa na wastani wa miaka 4 hadi 6 kuanza darasa la kwanza huku wakirushwa baadhi ya madarasa, hasa la saba na wangine wakitumia elimu ya nje kama Kenya na Uganda kusonga mbele katika vyuo vikuu vya huko.
Ila kwa wale tuliosoma Tanzania ni wazi kuwa kupata PhD si chini ya miaka 45, na kupata Uprofesa kama ngazi ya juu ya kielimu katika kufundisha inaweza kuchukua zaidi ya miaka 10 kwa Tanzania.Ukijumlisha na uchelevu wa kwenda shule huko nyuma wengi wanakuwa maprofesa bado miaka michache kustaafu. Hawa ndiyo magwiji walioiva.
Sasa kwa nini wameiva sasa, ndiyo tunawapa taarifa ya kusataafu!Hapa pana ulakini.Katika nchi za magharibi kustaafu ni miaka 65, na wengi huku wamepata PhD wakiwa chini ya miaka 25. Hivyo anaitumikia nchi yake kwa zaidi ya 30.
Ni wazi kuwa atarudisha fedha ya walipa kodi kwa kazi atakayoifanyia nchi yake.
Hasara yake ni kwamba wakati tumetumia pesa nyingi kuwasomesha katika vyuo vya nchi za magharibi kwa gharama zisizopungua milioni 100 kwa mtu mmoja kwa PhD tunamtumia chini ya miaka 10,kwa vile tu sheria inasema astaafu chini ya miaka 65!
Pesa nyingine zinakuja kama mikopo, hivyo hata mkopo haujalipwa na mtu hajaitumikia jamii yake anaambimwa astaafu kwa manufaa ya umma.
Ni sheria inapaswa kufuatwa. Lakini sheria hii kwa mmtazamo wangu nahisi ina matatizo na hasa kwa nchi yetu hii changa. Mbona Uingereza wanastaafu wakiwa na miaka 65.
Lengo kuu la sheria au taratibu za jamii yoyote ni kuwatumia jamii husika, sasa sheria hii inaonekana haina manufaa kwetu yatupasa kuijadili na kutafuta suluhu ya kudumu.
Rai yetu ni kwamba huu ni wakati muafaka wa kufikiria kuongeza kwa umri wa kustaafu iwe kwa hiyari au kwa manufaa ya umma umri uwe miaka 65.
Sunday, January 10, 2010
Bila walaji 'makini' ushiriki wetu u-mashakani
Gwiji wa Uchumi Profesa Michael Porter wa Chuo Kikuu cha Harvard katika nadharia yake maarufu kama 'Porter's Diamond Model' au 'faida ya ushindani'(Competitive Advantage) anabainisha wazi kuwa nchi ili ifanye vyema katika biashara ya kimataifa inahitaji kuwa na 'walaji makini'(Sophisticated Customers). Walaji wanaojua kuwa hii bidhaa haina ubora, na wapi waende ili wapate haki zao mara wanapokosa huduma bora toka kwa kampuni husika kwa 'uwongo' wa makusudi wa kibiashara.
Porter’s Diamond model inataja viashiria vikuu vinne vinavyo weza kufanya nchi iweze kushamiri katika biashara ya kimataifa, rasilimali (endowment factor),mahitaji ( demand condition), uhusiano wa kiviwanda (relating and supportive industries) na mbinu za kibiashara (firms strategy).
Makala haya itajadili umuhimu wa walaji makini kwa ustawi wa sekta ya kibiashara katika Tanzania na hasa viwanda. Tanzania inahaha kupanua wigo wake wa biashara ya nje, lakini wakati wote imekuwa haifanyi vyema.Kumekuwa na kauli mbiu za kila aina na taasisi kama CTI imekuja pia na kauli mbiu ya ‘kuwa mzalendo tumia bidhaa za nyumbani’
Kimsingi hakuna nchi iliyokuwa na kuimarika katika uchumi wake bila uchumi wa nchi husika kuimarika kwanza katika soko la ndani. Soko la ndani ni muhimu na mara zote limekuwa halina hadhari kubwa kama vile soko la kimataifa.
Tafiti fulani inabainisha kuwa kampuni nyingi zilizokwenda katika soko la kimataifa asilimia 50 zilianguka, kwa sababu mbalimbali. Pamoja na ukweli huo soko la kimataifa bado limebakia kuwa ni suluhu moja wapo ya kuimarika kwa uchumi si kwa nchi changa kama Tanzania tu bali hata nchi tajiri nazo zinahaha kuweza kujiimarisha katika masoko ya kimataifa mapya (Emerging markets) ya Asia na Afrika.
Sekta ya viwanda kwa sasa Tanzania ipo nyuma pamoja na mambo mengi inayoielemea sekta hii likiwemo uchakavu wa mitambo, miundo mbinu, ukosefu wa nishati(umeme wa mgao) lakini pia hili la kukosa walaji makini linasababisha kilio kwa viwanda vyetu.
Kwa mujibu wa Profesa Porter, soko la ndani linanafasi kubwa kwa kuchochea uhitaji wa bidhaa zenye ubora wa hali ya juu na hivyo kuipa changamoto kampuni katika kuinua na kuboresha bidhaa zake.
Ripoti ya Benki ya Tanazania(BoT) ya mwaka 2006/2007 inataja kuwa sekta ya viwanda imekuwa huku ikichangia pato la taifa kwa asilimia 9.2, ikiwa kuna mauzo ya nje kwa bidhaa za viwandani zenye thamani ya dola za kimarekani 226.8, huu ni mchupo wa dola milioni 34.6.
Mauzo yameimarika katika masoko ya Rwanda, Burundi na Kongo-Kinshasa kwa bidhaa za nguo kama vitenge na kangha, glasi, plasiti kukiwa na mafaniko toka kwa kiwanda cha Simba Plastiki inayouza katika nchi za SADC na pia viwanda vya chuma vinavyouza nondo.Uuzaji wa pombe kali kama konyagi na bia.
Ripoti hii haitaji kuhusu viwanda vya bidhaa za walaji kama sabuni na dawa za meno, lakini kuna taarifa za sabuni ya Foma Gold kufanya vizuri katika masoko ya Malawi na Zambia.
Pamoja na mafanikio haya tuliyojaribu kuyaorodhesha hapo juu, bado Tanzania inakaribiwa na mchango mdogo kutoka katika sekta ya viwanda vyake katika pato la taifa.
Mara zote kilio kimekekuwa kutoka miongoni mwa walaji na wazalishaji kuwa bidhaa za watanzania hazinunuliki sokoni.
Unaweza kujiuliza pamoja na kilio cha ubora mdogo wa bidhaa toka Uchina? Mbona bado tunagombania bidhaa hizo?Hii ni wazi kuwa walaji wa soko la Tanzania, siyo makini.
Ni walaji wanaoweza kununua kiatu cha plastiki kwa bei ya elfu 15000 toka Uchina na kuacha kiatu cha ngozi cha pale Moshi-Kilimanjaro.
Ni wazi kuwa mzalishaji wa kiatu naye atapunguza umakini hali ambayo itafanya kudorora kwa ubora wa bidhaa zake ili aweze kupambana na bidhaa feki za Uchina. Lakini kwa kufanya hivi ni wazi kuwa mbio hizi zinapunguza uwezo wetu katika kuyafikia masoko ya nje.
Ni walaji ambao hatuangalii ubora, ila tunajali uwingi na faida ya mlinganisho wa kifedha ya muda mfupi.
Mlaji makini anafahamu ubora wa bidhaa anayotaka kutumia kwa thamani ya fedha zake.Uhitaji wa bidhaa zenye ubora wa juu katika soko la ndani unavifanya viwanda husika kufikiri namna ya kuongeza jitihada katika tafiti zao(research and development)
Walaji wa Tanzania tunapokea kila kitu hatuko makini, hili linafanya viwanda vyetu vya ndani kubweteka na kusahau kuwa kuna siku za ushindani na hivyo ujio wa bidhaa toka nje zikipiga hodi.
Juhudi za kamisheni ya usawa wa biashara (FCC) za kuponda bidhaa mbovu zinazoingizwa nchini ni zenye kuungwa mkono kwani hizi bidhaa feki zinalemaza si tu walaji na wazalishaji pia.
Kabla ya Tanzania kuingia katika mfumo wa soko huria nadharia iliyokuwa imejengeka ni kuwa kwa vile ni serikali ndiyo mmiliki mkuu wa viwanda hivi hakuna namna ya kudhibiti, wala mteja hakuwa na nguvu ya kupinga bidhaa mbovu ikiwa imezalisha katika kiwanda cha umma.
Lakini imani yetu dhidi ya soko huria kuweza kutuletea bidhaa zenye ubora, imedimimizwa na ujio wa bidhaa feki.
Ni wazi kuwa sasa hivi tatizo ni walaji wasiolindwa wala kupata elimu juu ya umuhimu wa kiuchumi na kiusalama na afya wa kutumia bidhaa zenye ubora.
Ni ngumu kupata wateja walio makini kwa kutegemea nguvu za kiuchumi(soko) tu, yatupasa kuunda chama cha walaji. Chama cha walaji kitadai haki za walaji toka kwa watoa huduma hadi wazalishaji wa bidhaa.
Kwa kudai bidhaa zenye ubora ni wazi pia wazalishaji wa ndani wataamka na kuzalisha bidhaa zenye ubora kwa soko la nje pia.
Porter’s Diamond model inataja viashiria vikuu vinne vinavyo weza kufanya nchi iweze kushamiri katika biashara ya kimataifa, rasilimali (endowment factor),mahitaji ( demand condition), uhusiano wa kiviwanda (relating and supportive industries) na mbinu za kibiashara (firms strategy).
Makala haya itajadili umuhimu wa walaji makini kwa ustawi wa sekta ya kibiashara katika Tanzania na hasa viwanda. Tanzania inahaha kupanua wigo wake wa biashara ya nje, lakini wakati wote imekuwa haifanyi vyema.Kumekuwa na kauli mbiu za kila aina na taasisi kama CTI imekuja pia na kauli mbiu ya ‘kuwa mzalendo tumia bidhaa za nyumbani’
Kimsingi hakuna nchi iliyokuwa na kuimarika katika uchumi wake bila uchumi wa nchi husika kuimarika kwanza katika soko la ndani. Soko la ndani ni muhimu na mara zote limekuwa halina hadhari kubwa kama vile soko la kimataifa.
Tafiti fulani inabainisha kuwa kampuni nyingi zilizokwenda katika soko la kimataifa asilimia 50 zilianguka, kwa sababu mbalimbali. Pamoja na ukweli huo soko la kimataifa bado limebakia kuwa ni suluhu moja wapo ya kuimarika kwa uchumi si kwa nchi changa kama Tanzania tu bali hata nchi tajiri nazo zinahaha kuweza kujiimarisha katika masoko ya kimataifa mapya (Emerging markets) ya Asia na Afrika.
Sekta ya viwanda kwa sasa Tanzania ipo nyuma pamoja na mambo mengi inayoielemea sekta hii likiwemo uchakavu wa mitambo, miundo mbinu, ukosefu wa nishati(umeme wa mgao) lakini pia hili la kukosa walaji makini linasababisha kilio kwa viwanda vyetu.
Kwa mujibu wa Profesa Porter, soko la ndani linanafasi kubwa kwa kuchochea uhitaji wa bidhaa zenye ubora wa hali ya juu na hivyo kuipa changamoto kampuni katika kuinua na kuboresha bidhaa zake.
Ripoti ya Benki ya Tanazania(BoT) ya mwaka 2006/2007 inataja kuwa sekta ya viwanda imekuwa huku ikichangia pato la taifa kwa asilimia 9.2, ikiwa kuna mauzo ya nje kwa bidhaa za viwandani zenye thamani ya dola za kimarekani 226.8, huu ni mchupo wa dola milioni 34.6.
Mauzo yameimarika katika masoko ya Rwanda, Burundi na Kongo-Kinshasa kwa bidhaa za nguo kama vitenge na kangha, glasi, plasiti kukiwa na mafaniko toka kwa kiwanda cha Simba Plastiki inayouza katika nchi za SADC na pia viwanda vya chuma vinavyouza nondo.Uuzaji wa pombe kali kama konyagi na bia.
Ripoti hii haitaji kuhusu viwanda vya bidhaa za walaji kama sabuni na dawa za meno, lakini kuna taarifa za sabuni ya Foma Gold kufanya vizuri katika masoko ya Malawi na Zambia.
Pamoja na mafanikio haya tuliyojaribu kuyaorodhesha hapo juu, bado Tanzania inakaribiwa na mchango mdogo kutoka katika sekta ya viwanda vyake katika pato la taifa.
Mara zote kilio kimekekuwa kutoka miongoni mwa walaji na wazalishaji kuwa bidhaa za watanzania hazinunuliki sokoni.
Unaweza kujiuliza pamoja na kilio cha ubora mdogo wa bidhaa toka Uchina? Mbona bado tunagombania bidhaa hizo?Hii ni wazi kuwa walaji wa soko la Tanzania, siyo makini.
Ni walaji wanaoweza kununua kiatu cha plastiki kwa bei ya elfu 15000 toka Uchina na kuacha kiatu cha ngozi cha pale Moshi-Kilimanjaro.
Ni wazi kuwa mzalishaji wa kiatu naye atapunguza umakini hali ambayo itafanya kudorora kwa ubora wa bidhaa zake ili aweze kupambana na bidhaa feki za Uchina. Lakini kwa kufanya hivi ni wazi kuwa mbio hizi zinapunguza uwezo wetu katika kuyafikia masoko ya nje.
Ni walaji ambao hatuangalii ubora, ila tunajali uwingi na faida ya mlinganisho wa kifedha ya muda mfupi.
Mlaji makini anafahamu ubora wa bidhaa anayotaka kutumia kwa thamani ya fedha zake.Uhitaji wa bidhaa zenye ubora wa juu katika soko la ndani unavifanya viwanda husika kufikiri namna ya kuongeza jitihada katika tafiti zao(research and development)
Walaji wa Tanzania tunapokea kila kitu hatuko makini, hili linafanya viwanda vyetu vya ndani kubweteka na kusahau kuwa kuna siku za ushindani na hivyo ujio wa bidhaa toka nje zikipiga hodi.
Juhudi za kamisheni ya usawa wa biashara (FCC) za kuponda bidhaa mbovu zinazoingizwa nchini ni zenye kuungwa mkono kwani hizi bidhaa feki zinalemaza si tu walaji na wazalishaji pia.
Kabla ya Tanzania kuingia katika mfumo wa soko huria nadharia iliyokuwa imejengeka ni kuwa kwa vile ni serikali ndiyo mmiliki mkuu wa viwanda hivi hakuna namna ya kudhibiti, wala mteja hakuwa na nguvu ya kupinga bidhaa mbovu ikiwa imezalisha katika kiwanda cha umma.
Lakini imani yetu dhidi ya soko huria kuweza kutuletea bidhaa zenye ubora, imedimimizwa na ujio wa bidhaa feki.
Ni wazi kuwa sasa hivi tatizo ni walaji wasiolindwa wala kupata elimu juu ya umuhimu wa kiuchumi na kiusalama na afya wa kutumia bidhaa zenye ubora.
Ni ngumu kupata wateja walio makini kwa kutegemea nguvu za kiuchumi(soko) tu, yatupasa kuunda chama cha walaji. Chama cha walaji kitadai haki za walaji toka kwa watoa huduma hadi wazalishaji wa bidhaa.
Kwa kudai bidhaa zenye ubora ni wazi pia wazalishaji wa ndani wataamka na kuzalisha bidhaa zenye ubora kwa soko la nje pia.
Ni China au ni Afrika ambayo haiwezi kusema 'hapana'?
Katika siku za karibuni ongezeko la bidhaa 'feki' limekuwa ni tatizo kwa nchi nyingi zinazoendelea na Tanzania ikiwemo. Wakati wote huu Uchina imekuwa ikibeba lawama kuwa ndiyo mhusika na ni muendelezaji wa uuzaji wa bidhaa feki, kwa Afrika.
Niliwahi kuhudhruia sherehe moja ya harusi, nikashuhudia mama mmoja akipatwa na kadhia ya kuvunjika kwa kisigino cha kiatu chake cha ‘mchuchumio’ (High heels). Nilipomdadisi aliniambia kuwa ndiyo kwanza anakivaa(ulikuwa palo wa sare ya sherehe). Lakini alijifariji kuwa, amenunua 15000 tu, kariakoo.
Hasara ni hasara, je wale wanaounguliwa nyumba kwa kutumia nyaya au vifaa vyenye viwango vidogo!Ingawa ni ngumu kupata takwimu sahihi, lakini lililowazi ni kwamba miongoni mwetu tupo tunaopata hasara kwa kutumia bidhaa zenye viwango duni kutoka Uchina.
Tanzania bidhaa zenye ubora mdogo zinatusumbua. Makala haya itajaribu kutupia jicho hali ya kibiashara kati ya Uchina na Afrika.Lakini iweje katika maduka ya nchi za magharibi bidhaa za kichina zimejaa, lakini hawalalamiki kuwa kuna 'ufeki' kwa kiwango kama cha Tanzania?
Biashara kati ya Afrika na Uchina imeimarika kuanzia miaka ya 1990, huku Uchina ikiwa inaongoza kwa kufanya biashara na Afrika kwa miongoni mwa nchi za Asia, ikiwa na asilimia 39 ya biashara yake na Afrika.
Kutoshiri katika siasa za ndani za nchi za Afrika kunaifanya Uchina iwe kimbilio la bara hili.Hii ni sera ya mambo ya nje ya Uchina. Hivyo dikteta ana nafasi sawa na mlinda haki za binadamu mbele ya Uchina, ili mradi tu wao wanapata wanachohitaji na masilahi yao yanalindwa.
Biashara kati ya Afrika na Uchina imejikita zaidi katika , ujenzi wa miundo na usakaji wa malighafi hiki ikinunua mafuta kutoka Angola na Nigeria na Sudan. Ujio wa Uchina katika Afrika unahusishwa zaidi na kiu yake ya kusaka mafuta na maliasili zingine, huku ikiwa mtumiaji wa pili wa nishati ya mafuta baada ya Marekani ni wazi kuwa ni mshiriki mkubwa wa Afrika inayokidariwa kuwa na hifahdi ya asilimi 9 ya hifadhi ya mafuta ya Ulimweungu, lakini lenye kuvutia zaidi ni kuwa bara hili bado linaendelea kuvumbua vyanzo vingi vya mafuta katika maeneo mengi ya bara hili.
Jitihada za ushiriki wa Uchina unaimarishwa zaidi na jitihada zake za kufuta madeni ya bilioni 10 za kimarekani kwa nchi za Afrika. Ni wazi kuwa China ni mshiriki mzuri na mwenye kuangaliwa vyema katika kila analolifanya kwa maendeleo ya bara hili.
Kwa mujibu wa vyombo mbalimbali vya habari vya Uchina, Tanzania ni nchi inayoongoza katika Afrika kwa kupata misaada kutoka Uchina. Ni China ndiyo inayotoa mabilioni ya misaada katika kupiga’ jeki’ bajeti yetu na vyombo vya habari vimeripoti ‘mvua’ ya mabilioni ya mikopo kwa Tanzania katika siku za karibuni.
Misaada ipo kaitka kila kona, elimu, afya, jeshi, miundo mbinu nakadhalika. Ushiriki wa Uchina katika maendeleo ya Tanzania ni wa muda mrefu tangu (enzi zaMwalimu) awamu ya kwanza.
Urari wa kibiashara kati ya nchi hizi mbili upo chanya kwa China, huku ikiuza bidhaa zenye thamani ya dola milioni 128 na Tanzania ikiuza bidhaa zenye thamani ya dola milioni 6.62 kwa ripoti za mwaka 2002.
Kwa sasa biashara miongoni mwa nchi hizi mbili imeingiwa na mdudu ‘bidhaa feki’ huku Uchina ikipewa lawama, kwa kila bidhaa inayokamatwa na kila lalamiko katika Tanzania.
Wadadisi wa biashara za Uchina, wanabainisha kuwa ni ngumu kwa Uchina kudhibiti uzalishaji wa bidhaa hizi kwani baadhi ya majemedari wa jeshi wanamiliki au wanahisa katika baadhi ya viwanda.
Lakini, Uchina si muuzaji wa Afrika tu, akiwa na urari wa biashara wa zaidi ya dola 102 bilioni , ni muuzaji mkubwa katika masoko ya Ulaya na Marekani pia.Ni wazi kuwa kieneo si ni sehemu ndogo sana ya chumo lake biashara ya nje.
Tunachojiuliza ni kwa vipi bidhaa za kichina ziwepo kwa wingi na kutumiwa katika nchi kama Uingereza. Ufeki huku haupo kwa kiwango cha Tanzania?
Kamisheni ya Ushindani (FCC) inataja kuwa kiwi za milioni 20 na ‘tubelight’ za aina ya Phillips na Britimax zenye thamani ya dola 18000 zimeteketezwa mwaka 2007, kwa mujibu wa gazeti la Daily News la 1 May 2009.
Pia inakadiriwa kwa mwezi machi pekee 2008, bidhaa zenye thamani dola za kimarekani 224,000, ziliteketezwa na FCC. Ni wazi kuwa FCC kwa uchanga wake inafanya kazi kadiri inavyoweza ili kudhibiti bidhaa ‘feki’.
Vita hii inaonekana kwa sasa inasumbuliwa na ‘balkanization’ kila wizara na idara ya serikali ikipigana kutoka kivyake vyake. Kimsingi vita ya bidhaa feki ni ya jamii nzima, na bila chama cha walaji imara kinachoundwa na walaji wenyewe wafanya biashara wetu watandelea kujaza nchi yetu na bidhaa feki.
Vyombo vyenye mamalaka vimekuwa vingi hadi tuchanganyikiwa tuna TFDA, TBS, FCC.Walaji hatujui tukipata bidhaa ‘feki’ tuanzie wapi? Je tunaitambuaje bidhaa feki?Kuna muongozo wa viwango vya bidhaa, kuwa ubora wa bati unapaswa kuwa ni mchangayiko wa malighafi hizi kwa viwango anuai?Mlaji anayefahamu haya yote?Ni ngumu kwa baadhi ya mbinu kwa mlaji kuweza kutambua.
Ni wazi kuwa vita hii inahitaji kuongezewa nguvu na sheria inayowapa walaji nafasi ya kuwa na chama imara chenye kuwalinda tena chenye nguvu ya kulinda masilahi ya walaji.Katika nchi nyingi vyama hivi vipo na vimekuwa mwiba na vimefanikiwa kulinda nchi zao kuwa majalala ya bidhaa ‘bomu’ si toka nje tu hata wazalishaji wa ndani.
Vyama vya walaji(consumer Associations) vimekuwa vikiheshimiwa kuliko hata taasisi za serikali, kwa vile mara nyingi zimekuwa zikitoa taarifa bila kulinda masilahi ya kisiasa. Mfano mzuri ni imani ya waingereza juu ya FSA(Food Standard Agency) ni ndogo kwa vile ‘walibinya’ ukweli kuhusu homa ya kichaa cha ng’ombe (Bovine spongiform encephalopathy) kwa nia ya kulinda uchumi kwa gharama za walaji!
Ukiangalia mfano huu ni mingine sehemu zingine Duniani, utapata picha kwamba chama cha walaji kinahitajika zaidi kwa sasa Tanzania ili kulinda wateja katika siku za mfumo huu wa soko huria.Kwa sasa kuna chama cha kutetea wasafiria, hii ni hatua nzuri. Lakini yatupasa kukiimarisha chama hiki ili kiendelee kulinda manufaa ya walaji katika sekta ya usafairi.
Hii ni hatua moja tu kama nilivyosema, Tanzania ni kubwa na ushawishi wa wafanya biashara wetu katika kuleta na kufanikiwa kuingiza bidhaa feki unongeeka kila siku. Kwa mfano ukimwambia mteja kuwa ataweza kutambua bidhaa feki kwa tofauti ya jina(brand) hii inakosa nguvu sana kwani kwa sasa biashara ya Ulimwengu imejawa na wazuaji wa nembo zao(Own brand).
Hivyo tajiri anaweza kuagiza tani za vitasa toka Uchina akavipa jina la hardware yake. Ila hoja yetu ya ‘ufeki’ ipo katika malighafi zilizotumika kama zinakubarika katika soko la Tanzania.
Kwa kuangalia uwingi wa bidhaa za uchina katika nchi za magharibi na jinsi zinavyojipenyeza huko na kupapatikiwa na walaji kwa ‘upenyo’ wa bei ni wazi kuwa hatuna njia zaidi nasi pia kutumia bidhaa kutoka Uchina.
Ila kama nilivyokwisha kusema, hapa ni wauzaji wetu ndiyo walio kuwa na kasoro, ama hawana ufahamu na viwango vya nchi kwa bidhaa mbalimbali pale wanapoagiza. Suala la viwango vya ubora ni suala ‘tete’ na ni wazi kuwa viwango vya Tanzania, si sawa na Uingereza, ingawa kuna viwango vya bidhaa vya Ulimwengu, pia kuna nchi wanatumia viwango vyao bila hata kujali hivyo vya ulimwengu.
Hatuwatetei wajasiriamali ila yatupasa kupeleka elimu ya viwango kwa waaagizaji wa bidhaa toka nje, si kwa walaji tu. Inawezekana pia kati ya waagizaji ni wachahe wenye ufahamu juu ya viwango au kuona ‘muongozo’ wa viwango wa TBS, katika saketi inayotakiwa Tanzania iwe na ubora gani, kwa malighafi na uzito upi.
Pendekezo letu katika vita hii, mosi ni kuundwa kwa chama imara cha haki za walaji na pili kutungwa kwa sheria zenye kumpa mlaji haki za kiuchumi pale itakapogundulika kuwa bidhaa aliyotumia haikuwa na viwango husika,maana kwa sasa vinachomwa moto tu, vipi waliotumia wanapata malipo yoyote?Jibu ni kuwa hatupati
Pia tunapendekeza kutolewa kwa elimu ya viwango kwa waagizaji wa bidhaa toka nje ya nchi wafahamu kabla hatujawahukumu.
Ingawa Uchina ni mdau mkuu kwa maendeleo ya Tanzania kama nilivyokwisha kuonesha, yatupasa kuungana kama nchi kusema ‘HAPANA’ kwa bidhaa feki toka Uchina kwa masilahi ya nchi yetu. Tukiungana tunaweza.
Niliwahi kuhudhruia sherehe moja ya harusi, nikashuhudia mama mmoja akipatwa na kadhia ya kuvunjika kwa kisigino cha kiatu chake cha ‘mchuchumio’ (High heels). Nilipomdadisi aliniambia kuwa ndiyo kwanza anakivaa(ulikuwa palo wa sare ya sherehe). Lakini alijifariji kuwa, amenunua 15000 tu, kariakoo.
Hasara ni hasara, je wale wanaounguliwa nyumba kwa kutumia nyaya au vifaa vyenye viwango vidogo!Ingawa ni ngumu kupata takwimu sahihi, lakini lililowazi ni kwamba miongoni mwetu tupo tunaopata hasara kwa kutumia bidhaa zenye viwango duni kutoka Uchina.
Tanzania bidhaa zenye ubora mdogo zinatusumbua. Makala haya itajaribu kutupia jicho hali ya kibiashara kati ya Uchina na Afrika.Lakini iweje katika maduka ya nchi za magharibi bidhaa za kichina zimejaa, lakini hawalalamiki kuwa kuna 'ufeki' kwa kiwango kama cha Tanzania?
Biashara kati ya Afrika na Uchina imeimarika kuanzia miaka ya 1990, huku Uchina ikiwa inaongoza kwa kufanya biashara na Afrika kwa miongoni mwa nchi za Asia, ikiwa na asilimia 39 ya biashara yake na Afrika.
Kutoshiri katika siasa za ndani za nchi za Afrika kunaifanya Uchina iwe kimbilio la bara hili.Hii ni sera ya mambo ya nje ya Uchina. Hivyo dikteta ana nafasi sawa na mlinda haki za binadamu mbele ya Uchina, ili mradi tu wao wanapata wanachohitaji na masilahi yao yanalindwa.
Biashara kati ya Afrika na Uchina imejikita zaidi katika , ujenzi wa miundo na usakaji wa malighafi hiki ikinunua mafuta kutoka Angola na Nigeria na Sudan. Ujio wa Uchina katika Afrika unahusishwa zaidi na kiu yake ya kusaka mafuta na maliasili zingine, huku ikiwa mtumiaji wa pili wa nishati ya mafuta baada ya Marekani ni wazi kuwa ni mshiriki mkubwa wa Afrika inayokidariwa kuwa na hifahdi ya asilimi 9 ya hifadhi ya mafuta ya Ulimweungu, lakini lenye kuvutia zaidi ni kuwa bara hili bado linaendelea kuvumbua vyanzo vingi vya mafuta katika maeneo mengi ya bara hili.
Jitihada za ushiriki wa Uchina unaimarishwa zaidi na jitihada zake za kufuta madeni ya bilioni 10 za kimarekani kwa nchi za Afrika. Ni wazi kuwa China ni mshiriki mzuri na mwenye kuangaliwa vyema katika kila analolifanya kwa maendeleo ya bara hili.
Kwa mujibu wa vyombo mbalimbali vya habari vya Uchina, Tanzania ni nchi inayoongoza katika Afrika kwa kupata misaada kutoka Uchina. Ni China ndiyo inayotoa mabilioni ya misaada katika kupiga’ jeki’ bajeti yetu na vyombo vya habari vimeripoti ‘mvua’ ya mabilioni ya mikopo kwa Tanzania katika siku za karibuni.
Misaada ipo kaitka kila kona, elimu, afya, jeshi, miundo mbinu nakadhalika. Ushiriki wa Uchina katika maendeleo ya Tanzania ni wa muda mrefu tangu (enzi zaMwalimu) awamu ya kwanza.
Urari wa kibiashara kati ya nchi hizi mbili upo chanya kwa China, huku ikiuza bidhaa zenye thamani ya dola milioni 128 na Tanzania ikiuza bidhaa zenye thamani ya dola milioni 6.62 kwa ripoti za mwaka 2002.
Kwa sasa biashara miongoni mwa nchi hizi mbili imeingiwa na mdudu ‘bidhaa feki’ huku Uchina ikipewa lawama, kwa kila bidhaa inayokamatwa na kila lalamiko katika Tanzania.
Wadadisi wa biashara za Uchina, wanabainisha kuwa ni ngumu kwa Uchina kudhibiti uzalishaji wa bidhaa hizi kwani baadhi ya majemedari wa jeshi wanamiliki au wanahisa katika baadhi ya viwanda.
Lakini, Uchina si muuzaji wa Afrika tu, akiwa na urari wa biashara wa zaidi ya dola 102 bilioni , ni muuzaji mkubwa katika masoko ya Ulaya na Marekani pia.Ni wazi kuwa kieneo si ni sehemu ndogo sana ya chumo lake biashara ya nje.
Tunachojiuliza ni kwa vipi bidhaa za kichina ziwepo kwa wingi na kutumiwa katika nchi kama Uingereza. Ufeki huku haupo kwa kiwango cha Tanzania?
Kamisheni ya Ushindani (FCC) inataja kuwa kiwi za milioni 20 na ‘tubelight’ za aina ya Phillips na Britimax zenye thamani ya dola 18000 zimeteketezwa mwaka 2007, kwa mujibu wa gazeti la Daily News la 1 May 2009.
Pia inakadiriwa kwa mwezi machi pekee 2008, bidhaa zenye thamani dola za kimarekani 224,000, ziliteketezwa na FCC. Ni wazi kuwa FCC kwa uchanga wake inafanya kazi kadiri inavyoweza ili kudhibiti bidhaa ‘feki’.
Vita hii inaonekana kwa sasa inasumbuliwa na ‘balkanization’ kila wizara na idara ya serikali ikipigana kutoka kivyake vyake. Kimsingi vita ya bidhaa feki ni ya jamii nzima, na bila chama cha walaji imara kinachoundwa na walaji wenyewe wafanya biashara wetu watandelea kujaza nchi yetu na bidhaa feki.
Vyombo vyenye mamalaka vimekuwa vingi hadi tuchanganyikiwa tuna TFDA, TBS, FCC.Walaji hatujui tukipata bidhaa ‘feki’ tuanzie wapi? Je tunaitambuaje bidhaa feki?Kuna muongozo wa viwango vya bidhaa, kuwa ubora wa bati unapaswa kuwa ni mchangayiko wa malighafi hizi kwa viwango anuai?Mlaji anayefahamu haya yote?Ni ngumu kwa baadhi ya mbinu kwa mlaji kuweza kutambua.
Ni wazi kuwa vita hii inahitaji kuongezewa nguvu na sheria inayowapa walaji nafasi ya kuwa na chama imara chenye kuwalinda tena chenye nguvu ya kulinda masilahi ya walaji.Katika nchi nyingi vyama hivi vipo na vimekuwa mwiba na vimefanikiwa kulinda nchi zao kuwa majalala ya bidhaa ‘bomu’ si toka nje tu hata wazalishaji wa ndani.
Vyama vya walaji(consumer Associations) vimekuwa vikiheshimiwa kuliko hata taasisi za serikali, kwa vile mara nyingi zimekuwa zikitoa taarifa bila kulinda masilahi ya kisiasa. Mfano mzuri ni imani ya waingereza juu ya FSA(Food Standard Agency) ni ndogo kwa vile ‘walibinya’ ukweli kuhusu homa ya kichaa cha ng’ombe (Bovine spongiform encephalopathy) kwa nia ya kulinda uchumi kwa gharama za walaji!
Ukiangalia mfano huu ni mingine sehemu zingine Duniani, utapata picha kwamba chama cha walaji kinahitajika zaidi kwa sasa Tanzania ili kulinda wateja katika siku za mfumo huu wa soko huria.Kwa sasa kuna chama cha kutetea wasafiria, hii ni hatua nzuri. Lakini yatupasa kukiimarisha chama hiki ili kiendelee kulinda manufaa ya walaji katika sekta ya usafairi.
Hii ni hatua moja tu kama nilivyosema, Tanzania ni kubwa na ushawishi wa wafanya biashara wetu katika kuleta na kufanikiwa kuingiza bidhaa feki unongeeka kila siku. Kwa mfano ukimwambia mteja kuwa ataweza kutambua bidhaa feki kwa tofauti ya jina(brand) hii inakosa nguvu sana kwani kwa sasa biashara ya Ulimwengu imejawa na wazuaji wa nembo zao(Own brand).
Hivyo tajiri anaweza kuagiza tani za vitasa toka Uchina akavipa jina la hardware yake. Ila hoja yetu ya ‘ufeki’ ipo katika malighafi zilizotumika kama zinakubarika katika soko la Tanzania.
Kwa kuangalia uwingi wa bidhaa za uchina katika nchi za magharibi na jinsi zinavyojipenyeza huko na kupapatikiwa na walaji kwa ‘upenyo’ wa bei ni wazi kuwa hatuna njia zaidi nasi pia kutumia bidhaa kutoka Uchina.
Ila kama nilivyokwisha kusema, hapa ni wauzaji wetu ndiyo walio kuwa na kasoro, ama hawana ufahamu na viwango vya nchi kwa bidhaa mbalimbali pale wanapoagiza. Suala la viwango vya ubora ni suala ‘tete’ na ni wazi kuwa viwango vya Tanzania, si sawa na Uingereza, ingawa kuna viwango vya bidhaa vya Ulimwengu, pia kuna nchi wanatumia viwango vyao bila hata kujali hivyo vya ulimwengu.
Hatuwatetei wajasiriamali ila yatupasa kupeleka elimu ya viwango kwa waaagizaji wa bidhaa toka nje, si kwa walaji tu. Inawezekana pia kati ya waagizaji ni wachahe wenye ufahamu juu ya viwango au kuona ‘muongozo’ wa viwango wa TBS, katika saketi inayotakiwa Tanzania iwe na ubora gani, kwa malighafi na uzito upi.
Pendekezo letu katika vita hii, mosi ni kuundwa kwa chama imara cha haki za walaji na pili kutungwa kwa sheria zenye kumpa mlaji haki za kiuchumi pale itakapogundulika kuwa bidhaa aliyotumia haikuwa na viwango husika,maana kwa sasa vinachomwa moto tu, vipi waliotumia wanapata malipo yoyote?Jibu ni kuwa hatupati
Pia tunapendekeza kutolewa kwa elimu ya viwango kwa waagizaji wa bidhaa toka nje ya nchi wafahamu kabla hatujawahukumu.
Ingawa Uchina ni mdau mkuu kwa maendeleo ya Tanzania kama nilivyokwisha kuonesha, yatupasa kuungana kama nchi kusema ‘HAPANA’ kwa bidhaa feki toka Uchina kwa masilahi ya nchi yetu. Tukiungana tunaweza.
Monday, January 4, 2010
Sekta changa ya 'mboga mboga' na kitanzi cha VAT
Hivi karibuni Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imenukuliwa na Gazeti la Serikali Daily News la tarehe 26 Desemba 2009 kuwa limepitisha ‘tozo’ mpya ya kodi ya ongezeko la thamani ,VAT, kwa wauzaji wa masoko ya nje hata kama muuzaji ana pato lililochini ya milioni 40.
Mabadiliko haya yanatekelezwa kwa utetezi wa masilahi ya kulinda nchi hii ni kwa mujibu wa TRA. Safari hii VAT itatozwa hata kwa wale wajasiriamali wadogo, lakini tatizo si VAT, ila ni marejesho kuwa ‘yanabagua’. Kimsingi mlipaji wa VAT ni mlaji, kwani muuzaji hurejeshewa malipo yake, lakini hawa wadogo waliochini ya milioni 40 hawana cha ‘kurejeshewa’.
Tatizo hili la kukosa kuwarudishia ‘wajasiliamali’ ndiyo kiini cha makala haya. Tutajaribu kuangalia manufaa ya dhana hii kwa Taifa na pia tutatoa mchango wetu kuhusu hili.Ingawa tunaaamini hiki inawezekana ikawa ni kilio cha samaki machozi huenda na maji anaimba gwiji wa muziki wa dansi, Dr. Ramadhani Mtoro Ongala.Lakini tunaamini sauti yetu itasikika.
Kati ya sekta zilizoathirika na marekebisho haya ya kisheria ya VAT, ambayo kimsingi kamishina wa kodi ananguvu kisheria kuamaua nani alipe VAT ingawa sheria yenyewe ya inasema ni yule mwenye zaidi ya milioni 40.Sheria ya VAT kifungu sura ya 148 kifungu 19 kifungu kidogo 4, kinampa uwezo Kamishina wa Kodi kuamua nani alipe ingawa utakuwa upo chini ya milioni 40.
Ni vyema ikaeleweka wazi kuwa hatuna nia ya kujenga wala kutetea jamii ya watu wasio penda kulipa kodi, ila tunashaka na maamuzi haya kama kweli ya nia kuona nchi hii inang’ona ‘nanga’ kiuchumi.
Jitihada za kupambana na anguko la uchumi duniani imeona serikali nyingi zinahamasisha kuuza katika masoko ya nje, na zinatoa motisha ya punguzo la kodi kama si kufuta kabisa. Itakumbukwa pia katika siku za mwanzo za msukosuko huu kauli iliyokuwa inapigiwa chapuo na Marekani ni kuhakikisha nchi hazifungi mipaka yake ya kibiashara kwa kutumia njia kale (traditional barriers kama vile kodi za aina yoyote)
Ni kweli kuwa Tanzania inahaha ikitafuta kujinasua kutokana na msukosuko wa kiuchumi wa dunia kwa kutafuta kuongeza pato lake. Lakini kwa njia hii ya kutoza wauzaji wa nje na hasa wauzaji wa sekta changa ya mboga mboga ambayo imejawa na wazalisahjo wadogo wengi hauna mwisho mwema.
Sekta hii changa ya mboga mboga (horticulture) lakini katika makala haya tutajumlisha pia na floriculture, pale tutakoposema mboga mboga inakadiriwa tani kati ya 15 hadi 40 husafirishwa kwa wiki, kuelekea masoko ya ng’ambo kwa kutumia usafiri wa anga.
Hii ni bidhaa inayohitaji kufika sokoni haraka kutokana na tishio la kuharibika haraka (fast moving consumer goods). Kupitia chama chawazalishaji wa mboga mboga (TAHA) Tanzania ilijinyakulia tuzo ya shaba katika maonesho ya Amsterdam kwa mara ya kwanza wakati tukiwa washiriki kwa mara ya kwanza mwaka 2007.
Ikiwa inaleta chumo la dola milioni 50 kwa mwaka, na kuajiri watu wanaokadiriwa kufikia 10000, huku zaidi ya kampuni 20 zikiaminika kushiriki katika sekta hii. Ni wazi kuwa inahitaji kuangaliwa vizuri. Tanzania inakila sababu ya kuilinda sekta hii inayochipua kwa kuipa motisha lakini yanayotokea nchini ni kinyume chake.
Uzalishaji mkubwa wa mboga mboga upo Arusha, Kilimanjaro, lakini mikoa mingine kama Morogoro, Mbeya, Rukwa ,Tanga na Iringa nayo inafanya vyema na inakila hali ya kijiografia kuiwezesha kufanya vyema.
Mwenendo wa soko la ulimwengu wa mbogamboga katika nchi za Ulaya ni wenye kutia matumaini kwa siku za baadaye wa sekta hii nchini. Hii inatokana na ukweli kwamba katika Ulaya kuna mwamko wa kiafya kupinga ulaji wa nyama nyekundu kuanzia miaka ya kati ya sabini hali iliyopelekea kukubalika kwa nyama nyeupe kama kuku na nguruwe miongoni mwa watu wazee.
Uoga wa ulaji nyama ulishamiri zaidi baada ya kuibuka kwa ugonjwa kichaa za ng’ombe, BSE( Bovine spongiform encephalopathy) katika Uingereza miaka ya 1996.
Mwenendo wa soko umeimarika baada pia kuongezeka kwa hali ya kulinda wanyama, na ongezeko la walaji majani katika nchi hizi kwa imani za kisayansi. Kwa mfano tangu ongezeko la vitisho hivi soko la walaji wa nyama wa Uingereza umepungua ukiwa ni kilo 14.4 tu kwa mwaka.
Ni wazi kuwa Tanzania inazewa kunufaika na hakuna shaka kuwa sekta hii changa inahitaji kupigiwa ‘chapuo’ kuhakikisha kuwa tunakataa kuwa wauzaji wa wanunuzi wasio makini kama vile Kenya ambao hununua vitunguu na matunda toka kwetu kisha kuuza Ulaya kwa faida kubwa.
Hili la tozo ya VAT ya asilimia 18, ambapo hawa wadogo hawarejeshewi imevunja nguvu za wajasiriamali wanaohaha usiku na mchana kuona wanaunganishwa na soko la nje, na ni wazi kuwa si njia sahihi. Kwani Tanzania sasa hivi haihitaji kutoza kodi kubwa na hasa wauzaji wa nje ili kuongeza pato inahitaji kuhahakikisha wajasiriamali hawa wanauza katika soko la nje na wanapata suluhu katika mashaka yao.
Iweje wakubwa walio na pato kubwa la milioni zaidi ya 40 warudishiwe lakini wadogo wasirudishiwe? Hii si sawa. VAT analipa mlaji lakini safari hii wamekandamizwa wazalishaji tena wa sekta changa, kwa kigingi cha kulinda masilahi ya Taifa.Taifa gani linalolindwa wakati utekezaji wa sheria hii ni wazi kuwagawa watanzania, na hasa hawa wakulima wadogo wa mboga mboga!
Tanzania inavyanzo vingi vya kodi na tangu tumeamua kuchauga mabadiliko ya kiuchumi miaka ya 1980 ya soko huria, nia ilikuwa kuona utawala wa kodi unakuwa huru na wa haki.
Lakini safari hii tunaona kodi inakuwa kandamizi tena wakati wa hangaiko la Uchumi. Sekta hii ya mboga mboga nayo pia imepata msuko msuko, huku la soko la Uingereza likiwa limepungua kwa asilimia 20 kwa bidhaa toka Tanzania.Ni wazi kuwa sekta hii inahitaji kulindwa hasa ukizangatia kuwa ni wakulima wadogo ndiyo wanaoshiriki katika kuzalisha bidhaa hizi katika maeneo mengi nchini.
Kukosa pato kwa TRA kusihusishwe na kubinya walipa kodi waliojitoa na kukubali kulipa kodi kwa maendeleo ya Taifa. Na hili ndilo tatizo la Tanzania, mara zote nchi inakuwa iko mbele kuhakikisha inawakamua wale walipa kodi na si kuziba mianya ya uvujaji wa kodi.
Hivi karibuni gazeti la serikali Daily News la tarehe 20 Desmeba 2009, lilikuwa na taarifa kuwa wauzaji wa magogo na mbao nje ya nchi walikuwa wanataka kupunguzwa kwa kodi. Ombi ambalo serikali kupitia Waziri wa Viwanda na Biashara, Dr. Mary Nagu amekubali kulipokea na kuliona, huku Naibu wa Waziri wa Maliasili akilipigia ‘chapuo’ kuwa nchi inahitaji kupunguza tozo ya mbao na mazao mengine ya misitu ili kuongeza pato la taifa na hasa mauzo ya nje. Kwa sasa tozo ni 200,000/= kwa meta za ujazo.
Cha ajabu hapa tunapigia chapuo uvunaji wa maliasili ambayo ikivunwa ni hatari kuliko ikiachwa. Na wala hakuna anayeomba punguzo katika ‘mboga mboga’. Makala haya inaweka wazi kuwa Tanzania haiitaji kupunguza kodi kwa ajili ya mavuno ya misitu kama magogo na mbao, isipokuwa inahitaji kuweka ‘udhibiti’ ili kupambana na upotevu unaokisiwa kufikia dola milioni 58 za kimarekani kutokana na udanganyifu na utoroshaji wa mavuno ya misitu katika Asia na hasa Uchina.
Pia kuna eneo jingine nalo ni la uuzaji wa pombe kali(spirit) ambako TRA inaweza kuziba mianya ya upotevu na si kuwabinya wajasiriamali. Inakadiriwa zaidi ya bilioni 2 za kitanzania zinapotea kutokana na wakwepaji wa kodi wanaouza pombe kali. Na hivi karibuni kuna hawa wakurugenzi zaidi ya saba ambao TRA inawatafuta kwa kukwepa kodi ya uuzaji wa pombe kali.
Hatujitaji kupandisha kodi Tanzania ili tuweze kuendesha serkali yetu, changamoto ni katika kukusanya kodi kwa ufasaha na kwa uwazi.
Sekta ya mboga mboga inahitaji kung’oa nanga, ni vizuri ikiachwa ikue na ni vema kuiongezea motisha na si kuizima kila inapochipua. Chonde TRA angalieni mara mbili uamuzi wenu wa kutoza VAT ya asilimia 18 kwa mizigo inayosafirishwa kwa ndege nje ya nchi na wajasiriamali katika sekta ya mboga mboga.
Kwa sasa kuna madai kuwa wajasiriamali wameanza kutumia Kenya kusafirisha mizigo yao, ingawa hatuna takwimu za wazi, lakini kuna vitu tunapoteza. Njia ya Kenya haina mwisho mwema kwani mwaka 2007/2008 hasara ya bilioni moja ya kitanzania ilipatikana kutokana na kukatishwa kwa ruti kufuatia mapigano ya wenyewe kufuatia sintofahamu ya matokeo ya Uchaguzi.
Tunahitaji kufikira mara mbili katika kipindi hiki cha ‘msukosuko’ wa uchumi tunahitaji kupandisha kodi au kupunguza na hasa bidhaa tunazouza katika soko la nje. Jibu sahihi ni kwamba hatuhitaji kupandisha kodi kwa bidhaa za kilimo.
Yatupasa kuilinda sekta hii changa, kwa maendeleo ya watanzania na hasa waishio vijijini, ambao wanajishughulisha na uzalishaji wa mboga mboga. Na si kuwapigania wavuna magogo na wauza mbao.
Mabadiliko haya yanatekelezwa kwa utetezi wa masilahi ya kulinda nchi hii ni kwa mujibu wa TRA. Safari hii VAT itatozwa hata kwa wale wajasiriamali wadogo, lakini tatizo si VAT, ila ni marejesho kuwa ‘yanabagua’. Kimsingi mlipaji wa VAT ni mlaji, kwani muuzaji hurejeshewa malipo yake, lakini hawa wadogo waliochini ya milioni 40 hawana cha ‘kurejeshewa’.
Tatizo hili la kukosa kuwarudishia ‘wajasiliamali’ ndiyo kiini cha makala haya. Tutajaribu kuangalia manufaa ya dhana hii kwa Taifa na pia tutatoa mchango wetu kuhusu hili.Ingawa tunaaamini hiki inawezekana ikawa ni kilio cha samaki machozi huenda na maji anaimba gwiji wa muziki wa dansi, Dr. Ramadhani Mtoro Ongala.Lakini tunaamini sauti yetu itasikika.
Kati ya sekta zilizoathirika na marekebisho haya ya kisheria ya VAT, ambayo kimsingi kamishina wa kodi ananguvu kisheria kuamaua nani alipe VAT ingawa sheria yenyewe ya inasema ni yule mwenye zaidi ya milioni 40.Sheria ya VAT kifungu sura ya 148 kifungu 19 kifungu kidogo 4, kinampa uwezo Kamishina wa Kodi kuamua nani alipe ingawa utakuwa upo chini ya milioni 40.
Ni vyema ikaeleweka wazi kuwa hatuna nia ya kujenga wala kutetea jamii ya watu wasio penda kulipa kodi, ila tunashaka na maamuzi haya kama kweli ya nia kuona nchi hii inang’ona ‘nanga’ kiuchumi.
Jitihada za kupambana na anguko la uchumi duniani imeona serikali nyingi zinahamasisha kuuza katika masoko ya nje, na zinatoa motisha ya punguzo la kodi kama si kufuta kabisa. Itakumbukwa pia katika siku za mwanzo za msukosuko huu kauli iliyokuwa inapigiwa chapuo na Marekani ni kuhakikisha nchi hazifungi mipaka yake ya kibiashara kwa kutumia njia kale (traditional barriers kama vile kodi za aina yoyote)
Ni kweli kuwa Tanzania inahaha ikitafuta kujinasua kutokana na msukosuko wa kiuchumi wa dunia kwa kutafuta kuongeza pato lake. Lakini kwa njia hii ya kutoza wauzaji wa nje na hasa wauzaji wa sekta changa ya mboga mboga ambayo imejawa na wazalisahjo wadogo wengi hauna mwisho mwema.
Sekta hii changa ya mboga mboga (horticulture) lakini katika makala haya tutajumlisha pia na floriculture, pale tutakoposema mboga mboga inakadiriwa tani kati ya 15 hadi 40 husafirishwa kwa wiki, kuelekea masoko ya ng’ambo kwa kutumia usafiri wa anga.
Hii ni bidhaa inayohitaji kufika sokoni haraka kutokana na tishio la kuharibika haraka (fast moving consumer goods). Kupitia chama chawazalishaji wa mboga mboga (TAHA) Tanzania ilijinyakulia tuzo ya shaba katika maonesho ya Amsterdam kwa mara ya kwanza wakati tukiwa washiriki kwa mara ya kwanza mwaka 2007.
Ikiwa inaleta chumo la dola milioni 50 kwa mwaka, na kuajiri watu wanaokadiriwa kufikia 10000, huku zaidi ya kampuni 20 zikiaminika kushiriki katika sekta hii. Ni wazi kuwa inahitaji kuangaliwa vizuri. Tanzania inakila sababu ya kuilinda sekta hii inayochipua kwa kuipa motisha lakini yanayotokea nchini ni kinyume chake.
Uzalishaji mkubwa wa mboga mboga upo Arusha, Kilimanjaro, lakini mikoa mingine kama Morogoro, Mbeya, Rukwa ,Tanga na Iringa nayo inafanya vyema na inakila hali ya kijiografia kuiwezesha kufanya vyema.
Mwenendo wa soko la ulimwengu wa mbogamboga katika nchi za Ulaya ni wenye kutia matumaini kwa siku za baadaye wa sekta hii nchini. Hii inatokana na ukweli kwamba katika Ulaya kuna mwamko wa kiafya kupinga ulaji wa nyama nyekundu kuanzia miaka ya kati ya sabini hali iliyopelekea kukubalika kwa nyama nyeupe kama kuku na nguruwe miongoni mwa watu wazee.
Uoga wa ulaji nyama ulishamiri zaidi baada ya kuibuka kwa ugonjwa kichaa za ng’ombe, BSE( Bovine spongiform encephalopathy) katika Uingereza miaka ya 1996.
Mwenendo wa soko umeimarika baada pia kuongezeka kwa hali ya kulinda wanyama, na ongezeko la walaji majani katika nchi hizi kwa imani za kisayansi. Kwa mfano tangu ongezeko la vitisho hivi soko la walaji wa nyama wa Uingereza umepungua ukiwa ni kilo 14.4 tu kwa mwaka.
Ni wazi kuwa Tanzania inazewa kunufaika na hakuna shaka kuwa sekta hii changa inahitaji kupigiwa ‘chapuo’ kuhakikisha kuwa tunakataa kuwa wauzaji wa wanunuzi wasio makini kama vile Kenya ambao hununua vitunguu na matunda toka kwetu kisha kuuza Ulaya kwa faida kubwa.
Hili la tozo ya VAT ya asilimia 18, ambapo hawa wadogo hawarejeshewi imevunja nguvu za wajasiriamali wanaohaha usiku na mchana kuona wanaunganishwa na soko la nje, na ni wazi kuwa si njia sahihi. Kwani Tanzania sasa hivi haihitaji kutoza kodi kubwa na hasa wauzaji wa nje ili kuongeza pato inahitaji kuhahakikisha wajasiriamali hawa wanauza katika soko la nje na wanapata suluhu katika mashaka yao.
Iweje wakubwa walio na pato kubwa la milioni zaidi ya 40 warudishiwe lakini wadogo wasirudishiwe? Hii si sawa. VAT analipa mlaji lakini safari hii wamekandamizwa wazalishaji tena wa sekta changa, kwa kigingi cha kulinda masilahi ya Taifa.Taifa gani linalolindwa wakati utekezaji wa sheria hii ni wazi kuwagawa watanzania, na hasa hawa wakulima wadogo wa mboga mboga!
Tanzania inavyanzo vingi vya kodi na tangu tumeamua kuchauga mabadiliko ya kiuchumi miaka ya 1980 ya soko huria, nia ilikuwa kuona utawala wa kodi unakuwa huru na wa haki.
Lakini safari hii tunaona kodi inakuwa kandamizi tena wakati wa hangaiko la Uchumi. Sekta hii ya mboga mboga nayo pia imepata msuko msuko, huku la soko la Uingereza likiwa limepungua kwa asilimia 20 kwa bidhaa toka Tanzania.Ni wazi kuwa sekta hii inahitaji kulindwa hasa ukizangatia kuwa ni wakulima wadogo ndiyo wanaoshiriki katika kuzalisha bidhaa hizi katika maeneo mengi nchini.
Kukosa pato kwa TRA kusihusishwe na kubinya walipa kodi waliojitoa na kukubali kulipa kodi kwa maendeleo ya Taifa. Na hili ndilo tatizo la Tanzania, mara zote nchi inakuwa iko mbele kuhakikisha inawakamua wale walipa kodi na si kuziba mianya ya uvujaji wa kodi.
Hivi karibuni gazeti la serikali Daily News la tarehe 20 Desmeba 2009, lilikuwa na taarifa kuwa wauzaji wa magogo na mbao nje ya nchi walikuwa wanataka kupunguzwa kwa kodi. Ombi ambalo serikali kupitia Waziri wa Viwanda na Biashara, Dr. Mary Nagu amekubali kulipokea na kuliona, huku Naibu wa Waziri wa Maliasili akilipigia ‘chapuo’ kuwa nchi inahitaji kupunguza tozo ya mbao na mazao mengine ya misitu ili kuongeza pato la taifa na hasa mauzo ya nje. Kwa sasa tozo ni 200,000/= kwa meta za ujazo.
Cha ajabu hapa tunapigia chapuo uvunaji wa maliasili ambayo ikivunwa ni hatari kuliko ikiachwa. Na wala hakuna anayeomba punguzo katika ‘mboga mboga’. Makala haya inaweka wazi kuwa Tanzania haiitaji kupunguza kodi kwa ajili ya mavuno ya misitu kama magogo na mbao, isipokuwa inahitaji kuweka ‘udhibiti’ ili kupambana na upotevu unaokisiwa kufikia dola milioni 58 za kimarekani kutokana na udanganyifu na utoroshaji wa mavuno ya misitu katika Asia na hasa Uchina.
Pia kuna eneo jingine nalo ni la uuzaji wa pombe kali(spirit) ambako TRA inaweza kuziba mianya ya upotevu na si kuwabinya wajasiriamali. Inakadiriwa zaidi ya bilioni 2 za kitanzania zinapotea kutokana na wakwepaji wa kodi wanaouza pombe kali. Na hivi karibuni kuna hawa wakurugenzi zaidi ya saba ambao TRA inawatafuta kwa kukwepa kodi ya uuzaji wa pombe kali.
Hatujitaji kupandisha kodi Tanzania ili tuweze kuendesha serkali yetu, changamoto ni katika kukusanya kodi kwa ufasaha na kwa uwazi.
Sekta ya mboga mboga inahitaji kung’oa nanga, ni vizuri ikiachwa ikue na ni vema kuiongezea motisha na si kuizima kila inapochipua. Chonde TRA angalieni mara mbili uamuzi wenu wa kutoza VAT ya asilimia 18 kwa mizigo inayosafirishwa kwa ndege nje ya nchi na wajasiriamali katika sekta ya mboga mboga.
Kwa sasa kuna madai kuwa wajasiriamali wameanza kutumia Kenya kusafirisha mizigo yao, ingawa hatuna takwimu za wazi, lakini kuna vitu tunapoteza. Njia ya Kenya haina mwisho mwema kwani mwaka 2007/2008 hasara ya bilioni moja ya kitanzania ilipatikana kutokana na kukatishwa kwa ruti kufuatia mapigano ya wenyewe kufuatia sintofahamu ya matokeo ya Uchaguzi.
Tunahitaji kufikira mara mbili katika kipindi hiki cha ‘msukosuko’ wa uchumi tunahitaji kupandisha kodi au kupunguza na hasa bidhaa tunazouza katika soko la nje. Jibu sahihi ni kwamba hatuhitaji kupandisha kodi kwa bidhaa za kilimo.
Yatupasa kuilinda sekta hii changa, kwa maendeleo ya watanzania na hasa waishio vijijini, ambao wanajishughulisha na uzalishaji wa mboga mboga. Na si kuwapigania wavuna magogo na wauza mbao.
Subscribe to:
Posts (Atom)