Tanzania ni nchi ya kwanza Kusini mwa Jangwa la Sahara kuingizwa katika mpango wa ‘FAIR TRADE’(biashara huru), ila makala haya itatumia neno 'fair trade' moja kwa moja. Mpango huu ambao ulianza mwaka 1988 kupitia kahawa, kwa sasa unahusisha pia chai na samani hasa zenye kurembwa kwa shanga.
Kagera Cooperative Union (KCU) ni chama cha kwanza kunufaika na ‘Fair Trade’, kwa kuanza kuuza kahawa yake katika masoko ya Ulaya na Amerika. Kimsingi mpango huu umejikita katika nadharia ya kuwapa nguvu wakulima masikini wadogo wa nchi changa kuweza kufikia masoko ya Ulaya, huku wakinufaika kwa kazi ya jasho lao, kwa kulipwa bei nzuri ambazo ni zaidi ya bei ya soko la dunia.
Baada ya manufaa ya mpango huu kwa sasa nchini Tanzania vyama vya ushirika kama Karagwe District Cooperative Union, Kilimanjaro Native Cooperative Union pia wapo katika kuuza kahawa. Pia wafanyakazi wa mashamba ya chai katika Kibena ana Luponde Iringa na Lushoto, Tanga wapo katika mpango huu. Pia kuna mau yanayouzwa na kampuni ya Kiliflora ya Arusha kwa kutumia nembo ya 'Fairtrade' yakiwa chini ya Max Havelaar nembo inayoratibu masoko ya Uholanzi, Ubelgiji na Ufaransa.
Ili kufanikisha mpango wa fair trade ushirika imara ni muhimu kwa uhakika wa soko na mgawo wa pato la mauzo. Ushirika ndiyo kiunganishi kati ya wanunuzi na wakulima. Na hili la kuundwa kwa ushirika imara ni moja kati ya masharti makubwa ya kuweza kusajiliwa kama mzalishaji wa kahawa chini ya mpango wa 'fair trade'. Kwa wamiliki wa mashamba makubwa ya chai moja ya masharti ni kuundwa kwa vyama vya wafanya kazi huru vikiundwa na wafanyakazi wakipata hali bora kama huduma za kiafya na elimu kwa ajili ya watoto wao kutokana na chumo la 'Fair Trade'.
Mpango wa Fair Trade unashika kasi katika Afrika, Uganda na Malawi zinauza sukari, Kenya na Afrika Kusini zikijikita katika chai.Ingawa Tanzania ni mmoja kati ya wakongwe katika nchi za kusini mwa Jangwa la Sahara lakini ushiriki wake unaonekana kupungua. Na hii si kama bei ya kahawa au chai inaonekana kutengemaa sokoni la hasha.
Kwa mujibu wa mtafiti Profesa Fautini Karani Bee katika chapisho Fair Trade- Fair Future anabaisha wazi kwamba mauzo ya chama cha KNCU ya kahawa katika mpango huu, ni milioni 105, 069, 272, kwa mwaka 2008 wakati mwaka 2004 yalikuwa 175, 320, 894. Pato hili ni ile pesa ya ziada ambayo walaji wa Ulaya na Marekani wako tayari kulipa, achiliambali bei ya zao husika kuwa ipo juu ya bei ya soko.Ni wazi kuwa ushiriki wetu unalegalega.
Fair Trade imaleta hali bora kwa wakulima wadogo wa Tanzania , kuna wanafunzi zaidi ya 250 wamepata udhamini wa kupata elimu ya sekondari kupitia mpango uliobuniwa na chama cha KNCU. Pia washirika hawa wameweza kununua hisa katika Kilimanjaro Cooperative Bank.
Upepo wa mafanikio pia unavuma kwa washirika waliochini ya KCU ambao wameweza kununua hisa za kiwanda cha kahawa cha Kagera. Haya na mambo mengine mengi ni mafanikio ya juu wakulima wameweza kujipatia kupitia mfapongo huu.
Changamoto za Fair Trade katika Tanzanai ni nyingi , miongoni mwa hizo ni ukosefu wa vyama vya ushirika imara. Vyama vya ushirika ndiyo nyenzo ya Fair Trade, hivyo kufanya juhudi zote za kuondoa walanguzi sokoni kutegemea vyama hivi.
Wakulima wa Tanzania wamedhalilika na kuoenewa sana na vyama vya Ushirika. Ushirika umekuwa ni mzigo mzito kwa wakulima wa Tanzania. Ingawa ni kweli kuwa hakuna kesho bila kuwa na ushirika na hasa kwa wakulima wadogo na masikini wa Tanzania. Inashangaza ni kwanini serikali imekuwa na kauli nyingi bila vitendo!
Mtafiti Pirotte (2006) katika tafiti ‘Fair-Trade coffee in Nicaragua and Tanzania: a comparison’ iliyochapwa katika jarida la kisomi la Development in Practice , chapisho la 16 namba 5 anabainisha wazi kuwa wakulima sasa katika Tanzania, wamefikia hatua ya kuona FAIR TRADE, ni sawa na wafanyabiashara wengine (walanguzi), lakini hili limechangiwa zaidi na mwenendo wa ushirika. Ni wazi kuwa aliyeumwa na nyoka akiona unyasi atastuka. Maoni hayo yanaonesha wakulima walivyo kata tamaa na Ushirika hivyo lolote lilillochini yake ni wazi kuwa ni ulaghai!
Ni wazi kuwa mwenendo wa ushirika hauridhishi na wenye kuhitaji kurekebishwa ili kufikia lengo la kuwanufaisha wakulima wa Tanzania.
Hivi karibuni Waziri Mkuu M.K. P Pinda na Waziri wa Kilimo J. Wasira kwa nyakati tofauti wakiwa ziarani Japan na Vietnam wamesikika wakiweka wazi juu ya umuhimu wa ushirika imara kwa masilahi ya wakulima wa Tanzania.
Hili la kilio cha kukosa ushirika imara si jambo jipya. Ni kilio cha muda mrefu, na wala kauli za viongozi wetu katika kuhimiza ushirika imara si mpya pia.
Kauli za viongozi ni sahihi lakini zinahitaji vitendo katika kuwajengea wakulima imani dhidi ya ushirika na hili la Fair Trade linaonesha wazi jinsi tunavyochezea shilingi chooni.
Hali ya mambo inaonesha wazi kuwa kukosekana kwa ushirika imara Tanzania iko hatarini kupoteza nafasi yake katika kufikia masoko ya Marekani na Ulaya kupitia mpango huu. Mtafiti Paul Attontile anabainisha wazi kuwa mapungufu ya watendaji na viongozi wa ushirika yamewafanya hata wanunuzi wa kahawa chini ya mpango huu kufikiria kama kuna namna nyingine ya kuwafikia wakulima wadogo wa Tanzania.
Wakati Tanzania inalega lega kutumia nafasi hii, lakini nchi nyingine wao wako wanapambana kuongeza ushiriki wao kwa kusajili bidhaa nyingine mpya zilizoingizwa chini ya mfumo huu, kama vile asali, ndizi, nguo za pamba na bidhaa za mikono.
Mauzo ya sasa duniani kote ni zadi paundi 1.6 bilioni ukijumalisha masoko ya Ulaya na Amerika. Ingawa biashara ya Fair Trade ni wastani wa asilimia 1 ya biashara ya ulimwengu, lakini lenye kutia moyo ni kukua kwa kasi kwa biashara ya mauzo ya huku Itialia ikukua kwa asilimia 404 na Uingereza asilimia 72.
Walaji pia wa masoko ya Ulaya wako tayari kununua bidhaa zenye kujari masilahi ya wakulima masikini wa Kizio cha Kusini kwa zaidi ya asilimia 70. Mwenendo huu wa walaji na soko unaonesha kufanikiwa kwa mpango huu katika kulifikia soko na ‘kukuna’ nyoyo za walaji za ‘Trade not Aid’
Tuimarishe ushirika, kwani majuto ni mjukuu na Fair Trade imeonesha wazi kuwa inamwisho mwema kwa wakulima wa Tanzania, basi tusichezee shilingi chooni, shime viongozi wetu maneno matupu hayavunji mfupa.
Showing posts with label FAIR TRADE. Show all posts
Showing posts with label FAIR TRADE. Show all posts
Monday, March 29, 2010
Monday, March 1, 2010
Wakulima wadogo masikini watakombolewa na ‘fair trade’?
Ni mashamsham ya maazimisho ya wiki mbili ya kuhamasisha ‘fair trade’ katika nchi za Ulaya na Marekani kwa zaidi ya siku kumi na nne, toka Februari 22 hadi Machi 3. Miongoni mwa nchi zilizo katika mpango wa Fairtrade ni Uingereza, Ujerumani, Marekani, Japan,Ufaransa, Italia, Uholanzi, kuzitaja kwa uchahe tu. Kimsingi nchi hizi ndiyo masoko ya bidhaa za kilimo na za ubunifu wa mikono zinazotengenezwa katika nchi za Dunia ya tatu zikiingia sokoni kwa nembo ya fair trade.
Fair trade ni nadharia iliyojikita katika ‘utu’ huku ikiwa na msukumo wa kidini na maadili ili kuona wale watu waliomasikini kabisa duniani kutoka nchi masikini wanapata nafasi ya kufaidi jasho linalo tokana na kazi yao.Lengo kuu ni kuhakikisha bidhaa za watu wa kizio cha kusini zinafika katika masoko ya Ulaya na Amerika na wateja wakinunua bidhaa hizo ni wazi kuwa sehemu ya pato hurudi moja kwa moja katika nchi husika kusaidia maendeleo ya watu wa eneo hilo.
Nadharia hii inaweka katika vitendo, kile tunachokiita ‘trade not aid’. Lakini kwa sababu mfumo wa ulimwengu hauko wazi na bei za mazao mara zote zinaporomoka basi wakulima wa kizio cha kusini watapata nafuu, kwa kutoza bei ya juu kwa walaji wa kizio cha kaskazini na ile ziada iliyokuwa zaidi ya soko inakwenda kwa watu walio masikini.
Msukumo wa fair trade katika nchi za magharibi unaanzia katika makanisa, huku zaidi ya makanisa 6000 yakiwa yamejiunga katika mpango huu. Awali nimesema kuwa mpango huu umejikita katika maadili ya kiroho zaidi, na nyumba za ibada na taasisi za kidini na mashirika yao ndiyo yanayoongoza mpango huu wa ukombozi kwa watu wa kizio cha kusini.
Nguzo kuu ya maadili ya fairtrade yapo katika biblia, methali 13:23’Shamba la masikini hutoa mazao mengi , lakini bila haki hunyakuliwa’. Maneno hayo yamepamba baadhi ya makanisa katika Uingereza yanayojinadi kutumia bidhaa zenye nembo ya fair trade. Kupitia taasisi za kidini na mashirika yake wanaamini walaji wa nchi tajiri inabidi wanunue vitu kwa bei ya juu ili ziada irudi katika nchi asili ambako zao limelimwa ili kusaidia wakulima masikini.
Katika kutekeleza mpango huu njia moja wapo kuwa na chama cha ushirika na wakulima ujiunga pamoja kwa hiyari.Wakulima ni wale walio wadogo chini ya hekari 3 huku wakiwa wanaendesha shughuli zao za kilimo. Ingawa sasa kuna mjadala mkali wa kuangalia nini mantiki ya kutaka wakulima wadogo wapate haki ya kuuza kupitia mpango huu.
Inakadiriwa zaidi ya wakulima 500,000 na vyama vya ushirika 300 vipo katika mpango huu katika kizio cha kusini. Mauzo yanakadiriwa kufikia Euro bilioni 2.4 kwa mwaka jana.
Gazeti la The Independent la tarehe 25 Februari 2008 lilipoti mauzo ya bidhaa za fair trade kufikia paundi milioni 500 kwa Uingereza pekee. Huku idadi kubwa ya kampuni kubwa kama Mark Spencer, Waitrose,ASDA , Morrison na Tesco zikijiunga na kuahidi kuweka bidhaa za fairtrade katika maduka yao.
Fairtrade ni biashara inayovutia sana makampuni makubwa kwa sasa na kifimbo kinaonekana kupokonywa kutoka kwa taasisi za kihiyari kama Oxfarm, Traidcradt, Cafod sasa imekuwa ni biashara pendwa. Huu ni ushahidi wa wazi kuwa watu wengi wameitikia wito wa kununua kwa bei ya juu ili kwenda kusaidia watu masikini wa kizio cha kusini.
Tanzania inatajwa kama nchi ya kwanza kunufaika na mpango huu wa fairtrade, kwa kahawa kutoka Kagera mwaka 1988 kupitia chama cha Ushirika, Kagera Cooperative Union. Mpango huu pia unatumiwa na Kilimanjaro Native Cooperatives (KNCU) kwa kahawa yao kuuzwa Ulaya kupittia mpango huu.
Pia wamiliki wa mashamba ya chai wa Kibena, Iringa Tanzania ni miongozi mwa wafanyakazi wanaonufaika kwa bidhaa zao kufanikiwa kujipenyeza katika masoko ya Ulaya. Pia kuna bidhaa za mikono, zilizopo katika masoko ya Ulaya na Amerika kutoka Tanzania.
Mwenendo wa biashara unaonesha wazi kuzinufaisha nchi za dunia ya tatu. Tanzania kupitia KCU imeweza kuuza asilimia 7 ya kahawa yake yote inayozalisha. Kwa Mujibu ya mtandao wa taasisi ya Fair trade, inabainisha wazi kuwa wakulima wa Kagera wameweza kununua hisa za kiwanda cha Tanica kinachozalisha kahawa kwa asilimia 51.
Kahawa ya Arabica kutoka Afrika imewekwa katika bei ya dola 2.80 kwa Kilo,huku sent 11 dola za kimarekani kama bei ya juu (premium price) kwa kilo ikiwa fedha hii inapaswa kutumika kwa ajili ya maendeleo ya wakulima husika.
Bently W.R na wenzake katika Jarida la kisomi, Sustainable Development toleo 13, 2005 makala waliyoiita ‘What Tanzania’s farmers can teach the world’ wanabainisha kuwa kuna nyongeza ya kipato kwa wakulima wadogo wa kahawa wale walio katika mpango wa Fairtrade kulinganisha ni mifumo mingine .
Mafanikio mengine ni pale KNCU ilipoweza kuwalipia ada wanafunzi wanaokadiriwa kufikia 278, hawa ni wanafunzi wa shule za sekondari za serikali ambao wazazi wao wamefariki kwa ugonjwa wa Ukimwi au wanaoishi katika mazingira magumu.
Profesa Faustin K. Bee katika tafiti ‘Fair trade Fair futures: KNCU scholarship programme for children made vulnerable by AIDS’, 2009 anabaninsha wazi kuwa kipato cha kahawa kinachotokana na fairtrade kimekuwa si cha kuaminika kwa KNCU.Mwaka 2004 ilipatikana milioni 175 mwaka 2008 milioni 105. Majaaliwa ya mipango mizuri yote inawekwa majaribuni!
Haya ni mafanikio makubwa kufikiwa kwa wakulima wadogo waliojiunga chini ya chama cha ushirika. Lakini swali letu linabaki kuwa fairtrade ni mkombozi wa wakulima masikini toka mfumo mbovu wa biashara ya ulimwengu?Lililowazi ni kuwa fairtrade inaendeshwa nje ya nguvu za soko za ‘demand and supply’, kwani mlaji analipa zaidi ya bei ya soko na ziada inakwenda kwa wakulima wa nchi masikini.
Lililowazi kwamba wakulima wa Tanzania bado wanakumbukumbu ya maumivu ya walafi wachahce waliokula mali za ushirika bila kuchukuliwa hatua na safari hii fair trade inahimiza ushirika. Je Fair trade kupitia ushirika tutafikia lengo katika Tanzania, au yale yale?
Walaji wa Ulaya na Amerika hawatakuwa tayari kuona maadili ya utu yanavunjwa huku wao wakilipa bei ya juu kuliko bei ya soko na walafi wakihujumu chumo la fair trade. Ni wazi kuwa watasusa. Jukumu la kusukuma mbele malengo ya fair trade ni wazi kuwa Tanzania kama nchi ina nafasi kubwa ya kushiriki kuhakikisha wakulima wadogo wanalindwa na makucha ya walafi wanaojificha katika ushirika. Shime wenye mamlaka.
Fair trade ni nadharia iliyojikita katika ‘utu’ huku ikiwa na msukumo wa kidini na maadili ili kuona wale watu waliomasikini kabisa duniani kutoka nchi masikini wanapata nafasi ya kufaidi jasho linalo tokana na kazi yao.Lengo kuu ni kuhakikisha bidhaa za watu wa kizio cha kusini zinafika katika masoko ya Ulaya na Amerika na wateja wakinunua bidhaa hizo ni wazi kuwa sehemu ya pato hurudi moja kwa moja katika nchi husika kusaidia maendeleo ya watu wa eneo hilo.
Nadharia hii inaweka katika vitendo, kile tunachokiita ‘trade not aid’. Lakini kwa sababu mfumo wa ulimwengu hauko wazi na bei za mazao mara zote zinaporomoka basi wakulima wa kizio cha kusini watapata nafuu, kwa kutoza bei ya juu kwa walaji wa kizio cha kaskazini na ile ziada iliyokuwa zaidi ya soko inakwenda kwa watu walio masikini.
Msukumo wa fair trade katika nchi za magharibi unaanzia katika makanisa, huku zaidi ya makanisa 6000 yakiwa yamejiunga katika mpango huu. Awali nimesema kuwa mpango huu umejikita katika maadili ya kiroho zaidi, na nyumba za ibada na taasisi za kidini na mashirika yao ndiyo yanayoongoza mpango huu wa ukombozi kwa watu wa kizio cha kusini.
Nguzo kuu ya maadili ya fairtrade yapo katika biblia, methali 13:23’Shamba la masikini hutoa mazao mengi , lakini bila haki hunyakuliwa’. Maneno hayo yamepamba baadhi ya makanisa katika Uingereza yanayojinadi kutumia bidhaa zenye nembo ya fair trade. Kupitia taasisi za kidini na mashirika yake wanaamini walaji wa nchi tajiri inabidi wanunue vitu kwa bei ya juu ili ziada irudi katika nchi asili ambako zao limelimwa ili kusaidia wakulima masikini.
Katika kutekeleza mpango huu njia moja wapo kuwa na chama cha ushirika na wakulima ujiunga pamoja kwa hiyari.Wakulima ni wale walio wadogo chini ya hekari 3 huku wakiwa wanaendesha shughuli zao za kilimo. Ingawa sasa kuna mjadala mkali wa kuangalia nini mantiki ya kutaka wakulima wadogo wapate haki ya kuuza kupitia mpango huu.
Inakadiriwa zaidi ya wakulima 500,000 na vyama vya ushirika 300 vipo katika mpango huu katika kizio cha kusini. Mauzo yanakadiriwa kufikia Euro bilioni 2.4 kwa mwaka jana.
Gazeti la The Independent la tarehe 25 Februari 2008 lilipoti mauzo ya bidhaa za fair trade kufikia paundi milioni 500 kwa Uingereza pekee. Huku idadi kubwa ya kampuni kubwa kama Mark Spencer, Waitrose,ASDA , Morrison na Tesco zikijiunga na kuahidi kuweka bidhaa za fairtrade katika maduka yao.
Fairtrade ni biashara inayovutia sana makampuni makubwa kwa sasa na kifimbo kinaonekana kupokonywa kutoka kwa taasisi za kihiyari kama Oxfarm, Traidcradt, Cafod sasa imekuwa ni biashara pendwa. Huu ni ushahidi wa wazi kuwa watu wengi wameitikia wito wa kununua kwa bei ya juu ili kwenda kusaidia watu masikini wa kizio cha kusini.
Tanzania inatajwa kama nchi ya kwanza kunufaika na mpango huu wa fairtrade, kwa kahawa kutoka Kagera mwaka 1988 kupitia chama cha Ushirika, Kagera Cooperative Union. Mpango huu pia unatumiwa na Kilimanjaro Native Cooperatives (KNCU) kwa kahawa yao kuuzwa Ulaya kupittia mpango huu.
Pia wamiliki wa mashamba ya chai wa Kibena, Iringa Tanzania ni miongozi mwa wafanyakazi wanaonufaika kwa bidhaa zao kufanikiwa kujipenyeza katika masoko ya Ulaya. Pia kuna bidhaa za mikono, zilizopo katika masoko ya Ulaya na Amerika kutoka Tanzania.
Mwenendo wa biashara unaonesha wazi kuzinufaisha nchi za dunia ya tatu. Tanzania kupitia KCU imeweza kuuza asilimia 7 ya kahawa yake yote inayozalisha. Kwa Mujibu ya mtandao wa taasisi ya Fair trade, inabainisha wazi kuwa wakulima wa Kagera wameweza kununua hisa za kiwanda cha Tanica kinachozalisha kahawa kwa asilimia 51.
Kahawa ya Arabica kutoka Afrika imewekwa katika bei ya dola 2.80 kwa Kilo,huku sent 11 dola za kimarekani kama bei ya juu (premium price) kwa kilo ikiwa fedha hii inapaswa kutumika kwa ajili ya maendeleo ya wakulima husika.
Bently W.R na wenzake katika Jarida la kisomi, Sustainable Development toleo 13, 2005 makala waliyoiita ‘What Tanzania’s farmers can teach the world’ wanabainisha kuwa kuna nyongeza ya kipato kwa wakulima wadogo wa kahawa wale walio katika mpango wa Fairtrade kulinganisha ni mifumo mingine .
Mafanikio mengine ni pale KNCU ilipoweza kuwalipia ada wanafunzi wanaokadiriwa kufikia 278, hawa ni wanafunzi wa shule za sekondari za serikali ambao wazazi wao wamefariki kwa ugonjwa wa Ukimwi au wanaoishi katika mazingira magumu.
Profesa Faustin K. Bee katika tafiti ‘Fair trade Fair futures: KNCU scholarship programme for children made vulnerable by AIDS’, 2009 anabaninsha wazi kuwa kipato cha kahawa kinachotokana na fairtrade kimekuwa si cha kuaminika kwa KNCU.Mwaka 2004 ilipatikana milioni 175 mwaka 2008 milioni 105. Majaaliwa ya mipango mizuri yote inawekwa majaribuni!
Haya ni mafanikio makubwa kufikiwa kwa wakulima wadogo waliojiunga chini ya chama cha ushirika. Lakini swali letu linabaki kuwa fairtrade ni mkombozi wa wakulima masikini toka mfumo mbovu wa biashara ya ulimwengu?Lililowazi ni kuwa fairtrade inaendeshwa nje ya nguvu za soko za ‘demand and supply’, kwani mlaji analipa zaidi ya bei ya soko na ziada inakwenda kwa wakulima wa nchi masikini.
Lililowazi kwamba wakulima wa Tanzania bado wanakumbukumbu ya maumivu ya walafi wachahce waliokula mali za ushirika bila kuchukuliwa hatua na safari hii fair trade inahimiza ushirika. Je Fair trade kupitia ushirika tutafikia lengo katika Tanzania, au yale yale?
Walaji wa Ulaya na Amerika hawatakuwa tayari kuona maadili ya utu yanavunjwa huku wao wakilipa bei ya juu kuliko bei ya soko na walafi wakihujumu chumo la fair trade. Ni wazi kuwa watasusa. Jukumu la kusukuma mbele malengo ya fair trade ni wazi kuwa Tanzania kama nchi ina nafasi kubwa ya kushiriki kuhakikisha wakulima wadogo wanalindwa na makucha ya walafi wanaojificha katika ushirika. Shime wenye mamlaka.
Subscribe to:
Posts (Atom)