Soko la mazao la Tanzania tangu kuingia kwa kwa dhana ya soko huria vilio vya wakulima vimesikika kila kona. Hili halina nafasi katika makala haya kwani tunaamini mengi yamezungumzwa. Ila lililowazi ni kwamba tumeonesha jinsi wanunuzi wa korosho walivyokaidi agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika sehemu ya kwanza ya makala haya.
Tulishaonesha msimamo wetu katika makala yetu kuwa hatukubaliani na mawazo ya waheshimiwa wabunge kufuta stakabadhi ghalani pamoja na changamoto za sasa zilizopo katika zao la korosho.
Hebu tutupie jicho kidogo katika hoja zao mbili ambazo, mosi ni kuwa stakabadhi ghalani ni mfumo wakinyoyaji na pili unawatenaa wakulima wadogo.
Tuanze kwa kubainisha wazi kuwa si kweli kuwa mfumo wa stakabadhi ghalani ni kuwa wakinyonyaji. Isipokuwa ni mfumo ambao kinadharia unaleta uhuru wa kweli kwa wakulima wa nchi hii. Wakulima wa korosho wameshuhudia kulipwa katika mikupuo miwili na maeneo mengine mikupuo mitatu zaidi ya bei ya soko.
Wale waliouza korosho katika msimu wa mwaka jana kuna waliouza kwa kilo 650/= walichukua malipo yao na baadaye walilipwa mafao yao ya nyongeza ambayo baada ya kuuza korosho ilifikia kilo shilingi 800. Hivyo kufanya nyongeza ya zaidi ya shilingi mia kwa kilo.
Katika hali kama hii mkulima amenyonywa nini! Na liliwalowazi wale waliouza katika mtindo wa stakabadi ghalani walipata nafasi ya kujiwekea akiba kwa ajili ya pembejeo, lazima ieleweke watanzania walio wengi na hasa walio vijijini hawafaidi huduma za kibenki, hivyo kupitia stakabadhi ghalani wakulima wanaanza kuhifadhi kipato chao, kama vile mwenye akaunti, kwani hii ni ‘negotiable instrument’ inaweza kuthaminishwa. Hapa tunahitaji ubunifu katika sheria madhubuti katika kuhakikisha benki inapokea stakabadhi kama ‘inventory credit’.
Mfumo huu umeleta neema si katika korsho tu, hata katika kahawa , katika tafiti ya Gideon E. Onumah na Fedelis Temu ya mwaka 2005 katika kahawa na pamba iliyoitwa ‘Reducing Marketing Constraints and Enhancing Producer Income Through Warehouse System’ ilibaini kunufaika kwa wakulima wa Tarakea, Moshi kwa kipato kizuri kwa wanachama wa ushirika wa Tarakea ambao waliuza kahawa kwa kilo 1800/= tofauti na wenzao waliouza kwa mfumo wa soko huria wa kwa kilo 1250/=.
Ushirika hauchagui hivyo hoja ya kuwa mfumo huu unamtenga mkulima mdogo si sahihi. Ila ili mfumo huu usonge mbele unahitaji ushirika imara ambao umeundwa na wakulima wenyewe kwa ridhaa yao.
Mifano inaewza kuwa mingi kama vile IFAD inavyoshuhudia wakulima wa mahindi katika Karatu wanavyonufaika na mpango huu, huku wakiimarisha maisha yao. Mahindi yanauzwa 13,000/= kwa gunia wakati wa mavuno, lakini sasa wakulima wanaweka ghalani, wanuza hadi gunia la kilo mia 26,000/=.
Na lililowazi ni kwamba wengi wa kulima hawa ni wadogo walioungana kupitia ushirika wao kwa hiyari. Na wala hakuna tishio la kumnyonya mkulima mdogo. Sasa hili la kuwa stakabadhi ghalani ni tishio linatoka wapi?
Wataalmu wa biashara ya mazao wanabainisha kuwa mara zote adui mkubwa wa stakabadhi ghalani ni kilimo cha mikataba (Contract farming). Tanzania ina kampuni chache zinazofanya kilimo cha mikataba, kama vile Starbuck tena wapo katika kahawa wilayani Mbinga.
Inawezekana katika nchi yetu kilimo hiki kisiwe tishio kwa sasa ila yatupasa kuangalia namna yakufanya vyote viende kwa pamoja kwani vinamanufaa kwa wakulima wan nchi hii.
Pili upinzani wa stakabadhi ghalani unasababishwa na ‘bush buyers’ na kampuni za kinyonyaji zisizotaka kumuona mkulima anainuka. Hili ndilo lipo sana Tanzania.
Walanguzi wa korosho wapo wengi sana, wanakaa mjini msimu( Mwezi wa Kumi) ukifika kila mmoja na gunia la dagaa wa Mwanza au wa kigoma, chumvi na nguo za kichina au mitumba hujifanya wanauza kwa kubadirisha kwa korosho.
Hawa wananunua kwa kubadilishana ‘barter trade’. Ubaya wa biashara hii hutumia ‘kangomba’ (Ni kopo lenye kuingia kilo mbili na nusu) kubadilisha na mtumba au dagaa wa Mwanza wengi wame neemeka kupitia njia hii siyo rasimi.
Sasa hawa kwa vile ni watu waliokatiwa utamu bila jasho wanaona mwishowao unahatarishwa kwani sasa wakulima wamekombolewa, ndiyo wanaleta vitisho vya kuhamasiha kunyima kura wabunge na vurugu zote zile tulizo ziona katika makala haya sehemu ya kwanza chanzo ni hawa wanununzi wa ‘kangomba’.
Pia kampuni hizi za kihindi za ‘mfukoni’ zinamkono katika kuhimiza kuonekana kwa stakabadhi ghalani si mali kitu. Hizi kampuni zinafanya kazi kwa ‘ujanja ujanja’ Wengi wao kiukweli hawana mtaji, ila kinachotokea ni kwamba wao wanakubali kwenda vijijini na kujifanya wananunuzi kwa walau tofauti ya shilingi 20-100, ambayo wao huchukua kama cha juu. Hii biashara ya udalali imewanufaisha wengi hasa Mtwara Mjini.
Merehemu Profesa Seith Chachage anawaita makuadi wa soko huria. Na hawa nao hufanya kazi kupita mtindo huu wa soko huria kwa kusambaza vitisho.
Makuwadi hawa wanavyofanya ni unyonyaji ambao hauuvumiliki kama unaipenda nchi yako, kuna rafiki zangu walifanya kazi katika kampuni za korosho simulizi zao ni kwamba mkulima anapofika kuna madalali ambao wao wanijifanya ‘kumjua’ tajiri na bila wao ‘hauuzi’, sasa kwa vile mkulima ametoka Kitangari au Nambali hamjui tajiri wa kihindi anamkabidhi huyo ‘dalali’ kazi ya kufuatilia mauzo ya korosho zake.
Anazunguka anakuja na vijana ambao’ wanapiga’ bambo kutathimini ubora wa korosho kisha hudai kuwa ubora uko chini, hivyo hawawezi kununua.Hiki ni kitisho cha wazi. Mkulima amekodi gari na mjini siyo kwao, ataanza ‘kuweweseka’ tayari amekiwsha!
Wanauza korosho kwa bei kubwa na watachukua wao cha juu, kisha mkulima ataambulia maumivu, hawana huruma hata kidogo. Stakabadhi ghalani imewaondoa ndiyo hao ‘wanaugulia’ maumivu kwa kuleta hoja chakavu na hawa nao wananguvu ya kisiasa kwani wengi wao ni wapigaji wa ‘mdomo’ hasa vijiweni, basi wabunge wanajifanya kuleta hoja kuwa mfumo mbovu kumbe kutaka masilahi ‘uchwara’ yasiyo na tija, kwa walio wengi.
Changamoto ya kutolipa kwa wakati tumeshaona jitihada za serikali ilivyofuta madeni ya vyama vya ushirika ili viweze kukopesheka.Hili lilifanyika kwa baadhi ya vyama vya ushirika katika mkoa wa Mtwara na viliweza kupata mikopo kutoka benki ya CRDB. Ni wazi kuwa huu ni uamuzi mgumu na wa hali ya juu, ila yatupasa kwenda zaidi ya hapa.
Yatupasa kuhakikisha vyama vinakuwa na wataalmu wa kutosha, kwani katika ripoti ya mwaka 1967 ya Ushirika (Presidential Inquiry on Cooperative) mkoa wa Mtwara ulioneka kukosa wataalamu wa ushirika na masuala ya fedha. Ingawa muda ni mrefu lakini inawezekana kuwa tatizo hili mpaka leo lipo.
Lakini hili haliwezi kutufanya turudi nyuma. Wabunge lazima wabuni mbinu bora za kuhahakisha viongozi wanapata elimu ya kuweza kuendeleza ushirika katika maeneo yao
Pamoja na faida zake zote stakabadhi ghalani na hasa kwa Tanzania ina changamoto ambazo kimsingi tunapaswa kuzitafutia dawa na kitu kikubwa ni ubunifu.
Changamoto kubwa ni uhifadhi wa mazao, hapa tunazungumzia maghala yetu?Je yana bima? Ikitokea ghala limeshika moto, hatima ya mkulima wetu ikoje?
Kuhifadhi (Storage) ni taaluma, je tunawataalamu na mbinu za kutosha katika uhifadhi wa kisasa?
Nguvu ya stakabadhi tunayo mpatia mkulima wetu inakubalika katika taasisi zetu za kifedha kama ‘negotiable instruments’? Kama hapana tunaboreshaje?Kama ndiyo je uhalali wake ukoje kifedha?Sheria zetu zinasemaje kuhusu inventory credit?
Hatari nyingine ni kughushi (fraud) mara zote stakabadhi ghalani inaambatana na tatizo hili.
Ripoti moja ya Shirika la Umoja la Mataifa linaloshughulika na Chakula (FAO) inasema kama kilimo kinahitaji kuinua maisha na maendeleo kwa walio wengi basi mfumo imara wa mikopo unahitajika, na stakabadhi ghalani ni suluhu ya kudumu kwa wakulima kupata mikopo.
Tukijipanga na kuongeza ubunifu tunaweza.
Showing posts with label stakabadhi ghalani. Show all posts
Showing posts with label stakabadhi ghalani. Show all posts
Friday, November 6, 2009
Friday, October 30, 2009
Stakabadhi ghalani inahitaji ubunifu zaidi na si kusambaza 'woga'(SEHEMU YA KWANZA)
Siku chache zilizopita vyombo vya habari nchini viliripoti hoja ya kupinga kwa stakabadhi ghalani (warehouse receipt) toka kwa wabunge. Miongoni mwa wapinzani wa ‘stakabadhi ghalani’ ni Mheshimiwa Zito Zuberi Kabwe(Kigoma), Mohamed Sinani (Mtwara Mjini), Dustan Mkapa (Nanyumbu),Juma Abdalah Njwayo(Tandahimba) na Rainald Mrope (Masasi), Abdalah Mtutura (Tunduru) na Ibrahim Sanya (Mji Mkongwe).
Hoja yao ni kwamba stakabadhi ghalani ni mfumo wa ‘kinyonyaji’ kwa vile unamkopa mkulima, na kuna wanaodai kuwa mfumo huu ni wa kumtenga mkulima mdogo. Tunakiri kwamba mfumo huu ulipata upinzani mkubwa tangu kuasisiwa mkoani Mtwara.
Lakini upinzani wa safari hii umekuwa ni ‘mkali’ mno.Na linalotia shaka ni kuona kupungua kwa ‘ubunifu’ miongoni mwa viongozi katika kuboresha hali ya biashara ya mazao nchini.
Ubunifu (Innovation) ndiyo msingi mkuu wa mafanikio katika biashara ya ulimwengu wa leo. Biashara haihitaji tena woga,ila inahitaji kujitoa mhanga na kugeuza ‘woga’ kuwa changamoto huku ukifanikiwa kupitiwa changamoto.
Daima changamoto hazikosekani, na kwa mbunifu hizo ndizo chachu za kusonga mbele na si kurudi nyuma wala kukiri ‘kufeli’. Tanzania ya leo inahitaji viongozi wajasiriamali na si waoga ingawa kitu ni kizuri.
Kwa mfano Mheshimiwa Mrope anasema kuwa mkulima anakopwa na hapati malipo kwa wakati, hili linawezekana kutatuliwa tukijapanga na tukiongeza ‘ubunifu’. Hili haliwezi kutufanya kufuta mfumo huu.
Lingine linalotufanye tuone ni ‘uwoga’ wa kisiasa na kupungua kwa ubunifu ni hili la Mheshimiwa Njwayo.Mbunge Juma Abdalah Njwayo alichomewa nyumba yake mwaka juzi kisa alikuwa anatetea mfumo huu,leo hii ‘amebadilika’ hautaki kabisa!Nini kinamfanya mbunge huyu kubadilika ghafla namna hii? Ni kweli kuwa stakabadhi ghalani haifai na ni mfumo wa kinyonyaji kama anavyodai Mheshimiwa Dastan Mkapa?
Hatumaanishi kuwa Mheshimiwa Mbunge Juma Njwayo hakupaswa kubadilika, la hasha, ‘flexibility’ inakubalika katika nadharia za ‘kioungozi’ hasa baada ya kuona mapungufu ya kile ulichokuwa unaamni. Ila nadharia hii ya ‘kubadilika’ kimtizamo imejikita katika kutafuta ‘ukweli’ kabla ya kubadilka.
Hapa hatuzungumzii ukweli wa ‘kisiasa’ eti kwa vile 2010 yaja basi yapasa kusaka imani za wapiga kura. La hasha ni ukweli wa mwenendo wa kibiashara duniani na hasa biashara za mazao na hali ya wakulima wa nchi masikini.
Upinzani kwa mfumo huu wa ununuzi wa korosho haupo bungeni tu. Oktoba mosi mwaka 2007 wakulima wa Tandahimba waliandamana kupinga stakabadhi ghalani. Adnani Mbwana mwenyekiti wa Chama Cha Wakulima wa Korosho Tandahimba alipata hasara ya 1.8 milioni baada ya mikorosho yake kufyekwa.Kisa anaungama katika stakabadhi ghalani!
Naye mwenyekiti wa TANECU, Mbaraka Mjagama ni mhanga wa stakabadhi ghalani kwani nyumba yake ilibomolewa, (soma gazeti la habari leo 22,Oktoba.2007). Wapinga mfumo huu hawakuishia hapo kwani waliongeza kufuri katika maghala ili kudumaza jitihada za kuanza ununuzi wa korosho kupitia mfumo huu.
Mifano inaweza kuwa mingi kwani wanasiasa kama vile katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad naye alijitokeza kupinga mfumo huu soma gazeti la Tanzania Daima, 22.Oktoba. 2007.
Lenye kustaajabisha ni kwamba wakati Tandahimba wanakebehi na kupinga stakabadhi ‘ghalani’ wakulima wa pamba wanauomba kwa udi na uvumba. Wakulima katika wilaya za Getia na Kahama wanapigia chapuo mfumo huu uende katika pamba!
Mtu makini lazima atajiuliza mara mbili kwa nini korosho waupinge, pamba waulilie! Hawa wapamaba nini kinawafanya waulilie? Jibu rahisi ni kwamba wakulima wa pamba wamechoshwa na ‘kuhujumiwa’.
Tunaweka wazi msimamo wetu kwamba upinzani wa sasa wa stakabadhi ghalani ni kupungua kwa ‘ubunifu’ miongoni mwa viongozi wetu na ni dalili za kueneza hofu bila hata kupitia mwenendo mzima wa biashara ya mazao ya kilimo katika Tanzania.
Hivyo basi makala haya itatupia jicho mfumo huu, umuhimu wake kwa wakulima wa nchi hii, chagamoto zake na kushauri nini kifanyike katika siku za baadae ili kuboresha biashara ya mazao katika Tanzania.
Stakabadhi ghalani (warehouse receipt) ni nini?Si mfumo mpya duniani, wataalamu wa historia ya biashara wanabainisha kuwa ulianza katika Mesopotamia, na ulikua na kushamiri katika Marekani katika karne ya kumi na nane. Sheria ya kwanza imara na madhubuti kuhusu stakabadhi ghalani ilipitishwa katika Marekani mwaka 1916.
Asili ya stakabadhi ghalani ni nini?stakabadhi ghalani hutumika hasa katika kilimo, ni mfumo ambao umeibuliwa ili kuweza kupunguza kuyumba kwa bei ya mazao ya kilimo (price volatility) hasa wakati wa mavuno, na kumsababishia mkulima hasara kubwa na umasikini ambao huwa unamzunguka daima dumu.
Kutokana na kukosa bei ya uhakika wa mazao mara zote kilimo kimekuwa hakikopesheki, na hatari ‘risk’ kwa mikopo ya kilimo imekuwa ni kubwa na mara zote benki zimekuwa zikionesha kisogo sekta hii.
Hili likafanya nadharia ya stakabadhi ghalani kuchipuka Duniani nia ikiwa kumpatia mkulima bei yenye kuridhisha.Mara baada ya kusambaratika kwa jumuiya ya Ki-Soviet nchi za Ulaya Mashariki nazo zilijikuta haziwezi tena kulinda wakulima wake. Nchi kama Bulgaria, Kazakhstani, Hangari, Slovakia na Lithuania ni miongoni mwa vinara wa stakabadhi ghalani na wanaitumia huku wakulima wakineemeka.
Pia wakati wa kudorora kwa bei ya mazao ndiyo ulikuwa wakati wa ‘bush buyers’ walanguzi kujipenyeza na kununua kwa ‘lumbesa’ au ‘kangomba’. Nalo hili stakabadhi ghalani imelidhibiti. Taarifa za karibuni zinaonesha kuhimarika kwa ubora wa korosho.
Kimsingi mkulima hupewa hati mara baada ya kuuza mazao yake kwa ushirika, na malipo ya kati ya asilimia 65-70 hufanyika. Na mara zote sehemu iliyobaki hutegemea mauzo yake kwa wafanya biashara wanaonunua; safari hii hawakutani na mkulima bali ushirika, na si tena gunia moja bali ni tani zilizokusanywa pamoja.
Uwezo kwa kujadili bei umeongezeka kutegemeana na ushirika imara. Ila kubwa zaidi ni kwamba hati ya mauzo yaliyo ghalani ni ‘pesa’. Ina nguvu kama ‘negotiable instruments’ kutegemeana na sheria za nchi husika. Katika nchi zilizoendelea stakabadhi inayotolewa na ghala la serikali ndiyo huwa yenyekuaminika zaidi. Benki ya Dunia inasema hadi miaka kumi wakulima wa nchi za Ulaya Mashariki huweka mazao yao ghalani, huku wakiwinda bei nzuri!
Tafiti fulani iliyofanywa katika Tanzania na Zambia inataja wanunuzi wa mazao( bush buyers) hujipatia faida ya 70 asilimia na huku wakitumia gharama za kuhifadhi kwa 25 asimilia ya bei ya kununulia baada ya muda wa miezi miwili tu toka msimu wa mavuno.
Katika Tanzania stakabadhi ghalani imeingia baada ya upembuzi ya kinifu uliofanywa na Taasisi ya Maliasili( Natural Resource Institute) ya Chuo Kikuu cha Greenwich nchini Uingereza. Tafiti hii ilifanyika katika Zambia na Uganda pia katika miaka ya 1990 na kukamilika mwaka 1997.Na mazao ya kujaribia nadharia hii yalianza kama Kahawa na Korosho. Ndipo fuko la Common Fund for Commodities lilipotoa chagizo la kuundwa kwa stakabadhi ghalani na sheria ya kwanza ilikuwa June 2005 ilifikishwa Bungeni (unaweza kutembelea www.nri.org/project)
Msimu wa ununzi wa korosho wa 2007 ulishuhudia kuanza kwa mfumo huu, ikiwa ni kivuli cha kugoma kwa kampuni za kununua korosho zilizokuwa zinanunua chini ya bei ya makubaliano.
Kampuni hizi zilipinga agizo la Rais Jakaya Kikwete, kampuni sita zilinyang’anywa leseni. Hili la kupinga agizo la Rais ni fedheha kwa nchi, na utatuzi wake lazima uwe wa kisayansi na hapo ndipo ‘stakabadhi ghalani’ inachipuka.
Serikali haikuleta mfumo huu kama ubabaishaji tu, la hasha, kwani ni kilio cha wakulima wenyewe dhidi ya uonevu wa kampuni za ununuzi wa korosho, leo hii inatushangaza kusikia kuwa wawakilishi wa wananchi( wabunge) wanataka kuundoa mfumo huu.
Wanataka kuturudisha wapi? Kule tulikotoka, kwa wafanya biashara wahuni na wevi. Hata kidogo.
Lakini lililowazi ni kwamba tumeona kuwa mfumo huu hauna muda mrefu nchini na unalengo la kumlinda mkulima wa Tanzania. Basi yatupasa kutupia jicho hizo changamoto zinazoletwa na wapinzani wa stakabadhi ghalani pia tutatoa maoni yetu jinsi ya kuzikabili na kuona mifano halisi ya mafanikio ya stakabadhi ghalani si Tanzania tu pia katika nchi za Ulaya Mashariki ambako mfumo huu unatumika pia.
Hoja yao ni kwamba stakabadhi ghalani ni mfumo wa ‘kinyonyaji’ kwa vile unamkopa mkulima, na kuna wanaodai kuwa mfumo huu ni wa kumtenga mkulima mdogo. Tunakiri kwamba mfumo huu ulipata upinzani mkubwa tangu kuasisiwa mkoani Mtwara.
Lakini upinzani wa safari hii umekuwa ni ‘mkali’ mno.Na linalotia shaka ni kuona kupungua kwa ‘ubunifu’ miongoni mwa viongozi katika kuboresha hali ya biashara ya mazao nchini.
Ubunifu (Innovation) ndiyo msingi mkuu wa mafanikio katika biashara ya ulimwengu wa leo. Biashara haihitaji tena woga,ila inahitaji kujitoa mhanga na kugeuza ‘woga’ kuwa changamoto huku ukifanikiwa kupitiwa changamoto.
Daima changamoto hazikosekani, na kwa mbunifu hizo ndizo chachu za kusonga mbele na si kurudi nyuma wala kukiri ‘kufeli’. Tanzania ya leo inahitaji viongozi wajasiriamali na si waoga ingawa kitu ni kizuri.
Kwa mfano Mheshimiwa Mrope anasema kuwa mkulima anakopwa na hapati malipo kwa wakati, hili linawezekana kutatuliwa tukijapanga na tukiongeza ‘ubunifu’. Hili haliwezi kutufanya kufuta mfumo huu.
Lingine linalotufanye tuone ni ‘uwoga’ wa kisiasa na kupungua kwa ubunifu ni hili la Mheshimiwa Njwayo.Mbunge Juma Abdalah Njwayo alichomewa nyumba yake mwaka juzi kisa alikuwa anatetea mfumo huu,leo hii ‘amebadilika’ hautaki kabisa!Nini kinamfanya mbunge huyu kubadilika ghafla namna hii? Ni kweli kuwa stakabadhi ghalani haifai na ni mfumo wa kinyonyaji kama anavyodai Mheshimiwa Dastan Mkapa?
Hatumaanishi kuwa Mheshimiwa Mbunge Juma Njwayo hakupaswa kubadilika, la hasha, ‘flexibility’ inakubalika katika nadharia za ‘kioungozi’ hasa baada ya kuona mapungufu ya kile ulichokuwa unaamni. Ila nadharia hii ya ‘kubadilika’ kimtizamo imejikita katika kutafuta ‘ukweli’ kabla ya kubadilka.
Hapa hatuzungumzii ukweli wa ‘kisiasa’ eti kwa vile 2010 yaja basi yapasa kusaka imani za wapiga kura. La hasha ni ukweli wa mwenendo wa kibiashara duniani na hasa biashara za mazao na hali ya wakulima wa nchi masikini.
Upinzani kwa mfumo huu wa ununuzi wa korosho haupo bungeni tu. Oktoba mosi mwaka 2007 wakulima wa Tandahimba waliandamana kupinga stakabadhi ghalani. Adnani Mbwana mwenyekiti wa Chama Cha Wakulima wa Korosho Tandahimba alipata hasara ya 1.8 milioni baada ya mikorosho yake kufyekwa.Kisa anaungama katika stakabadhi ghalani!
Naye mwenyekiti wa TANECU, Mbaraka Mjagama ni mhanga wa stakabadhi ghalani kwani nyumba yake ilibomolewa, (soma gazeti la habari leo 22,Oktoba.2007). Wapinga mfumo huu hawakuishia hapo kwani waliongeza kufuri katika maghala ili kudumaza jitihada za kuanza ununuzi wa korosho kupitia mfumo huu.
Mifano inaweza kuwa mingi kwani wanasiasa kama vile katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad naye alijitokeza kupinga mfumo huu soma gazeti la Tanzania Daima, 22.Oktoba. 2007.
Lenye kustaajabisha ni kwamba wakati Tandahimba wanakebehi na kupinga stakabadhi ‘ghalani’ wakulima wa pamba wanauomba kwa udi na uvumba. Wakulima katika wilaya za Getia na Kahama wanapigia chapuo mfumo huu uende katika pamba!
Mtu makini lazima atajiuliza mara mbili kwa nini korosho waupinge, pamba waulilie! Hawa wapamaba nini kinawafanya waulilie? Jibu rahisi ni kwamba wakulima wa pamba wamechoshwa na ‘kuhujumiwa’.
Tunaweka wazi msimamo wetu kwamba upinzani wa sasa wa stakabadhi ghalani ni kupungua kwa ‘ubunifu’ miongoni mwa viongozi wetu na ni dalili za kueneza hofu bila hata kupitia mwenendo mzima wa biashara ya mazao ya kilimo katika Tanzania.
Hivyo basi makala haya itatupia jicho mfumo huu, umuhimu wake kwa wakulima wa nchi hii, chagamoto zake na kushauri nini kifanyike katika siku za baadae ili kuboresha biashara ya mazao katika Tanzania.
Stakabadhi ghalani (warehouse receipt) ni nini?Si mfumo mpya duniani, wataalamu wa historia ya biashara wanabainisha kuwa ulianza katika Mesopotamia, na ulikua na kushamiri katika Marekani katika karne ya kumi na nane. Sheria ya kwanza imara na madhubuti kuhusu stakabadhi ghalani ilipitishwa katika Marekani mwaka 1916.
Asili ya stakabadhi ghalani ni nini?stakabadhi ghalani hutumika hasa katika kilimo, ni mfumo ambao umeibuliwa ili kuweza kupunguza kuyumba kwa bei ya mazao ya kilimo (price volatility) hasa wakati wa mavuno, na kumsababishia mkulima hasara kubwa na umasikini ambao huwa unamzunguka daima dumu.
Kutokana na kukosa bei ya uhakika wa mazao mara zote kilimo kimekuwa hakikopesheki, na hatari ‘risk’ kwa mikopo ya kilimo imekuwa ni kubwa na mara zote benki zimekuwa zikionesha kisogo sekta hii.
Hili likafanya nadharia ya stakabadhi ghalani kuchipuka Duniani nia ikiwa kumpatia mkulima bei yenye kuridhisha.Mara baada ya kusambaratika kwa jumuiya ya Ki-Soviet nchi za Ulaya Mashariki nazo zilijikuta haziwezi tena kulinda wakulima wake. Nchi kama Bulgaria, Kazakhstani, Hangari, Slovakia na Lithuania ni miongoni mwa vinara wa stakabadhi ghalani na wanaitumia huku wakulima wakineemeka.
Pia wakati wa kudorora kwa bei ya mazao ndiyo ulikuwa wakati wa ‘bush buyers’ walanguzi kujipenyeza na kununua kwa ‘lumbesa’ au ‘kangomba’. Nalo hili stakabadhi ghalani imelidhibiti. Taarifa za karibuni zinaonesha kuhimarika kwa ubora wa korosho.
Kimsingi mkulima hupewa hati mara baada ya kuuza mazao yake kwa ushirika, na malipo ya kati ya asilimia 65-70 hufanyika. Na mara zote sehemu iliyobaki hutegemea mauzo yake kwa wafanya biashara wanaonunua; safari hii hawakutani na mkulima bali ushirika, na si tena gunia moja bali ni tani zilizokusanywa pamoja.
Uwezo kwa kujadili bei umeongezeka kutegemeana na ushirika imara. Ila kubwa zaidi ni kwamba hati ya mauzo yaliyo ghalani ni ‘pesa’. Ina nguvu kama ‘negotiable instruments’ kutegemeana na sheria za nchi husika. Katika nchi zilizoendelea stakabadhi inayotolewa na ghala la serikali ndiyo huwa yenyekuaminika zaidi. Benki ya Dunia inasema hadi miaka kumi wakulima wa nchi za Ulaya Mashariki huweka mazao yao ghalani, huku wakiwinda bei nzuri!
Tafiti fulani iliyofanywa katika Tanzania na Zambia inataja wanunuzi wa mazao( bush buyers) hujipatia faida ya 70 asilimia na huku wakitumia gharama za kuhifadhi kwa 25 asimilia ya bei ya kununulia baada ya muda wa miezi miwili tu toka msimu wa mavuno.
Katika Tanzania stakabadhi ghalani imeingia baada ya upembuzi ya kinifu uliofanywa na Taasisi ya Maliasili( Natural Resource Institute) ya Chuo Kikuu cha Greenwich nchini Uingereza. Tafiti hii ilifanyika katika Zambia na Uganda pia katika miaka ya 1990 na kukamilika mwaka 1997.Na mazao ya kujaribia nadharia hii yalianza kama Kahawa na Korosho. Ndipo fuko la Common Fund for Commodities lilipotoa chagizo la kuundwa kwa stakabadhi ghalani na sheria ya kwanza ilikuwa June 2005 ilifikishwa Bungeni (unaweza kutembelea www.nri.org/project)
Msimu wa ununzi wa korosho wa 2007 ulishuhudia kuanza kwa mfumo huu, ikiwa ni kivuli cha kugoma kwa kampuni za kununua korosho zilizokuwa zinanunua chini ya bei ya makubaliano.
Kampuni hizi zilipinga agizo la Rais Jakaya Kikwete, kampuni sita zilinyang’anywa leseni. Hili la kupinga agizo la Rais ni fedheha kwa nchi, na utatuzi wake lazima uwe wa kisayansi na hapo ndipo ‘stakabadhi ghalani’ inachipuka.
Serikali haikuleta mfumo huu kama ubabaishaji tu, la hasha, kwani ni kilio cha wakulima wenyewe dhidi ya uonevu wa kampuni za ununuzi wa korosho, leo hii inatushangaza kusikia kuwa wawakilishi wa wananchi( wabunge) wanataka kuundoa mfumo huu.
Wanataka kuturudisha wapi? Kule tulikotoka, kwa wafanya biashara wahuni na wevi. Hata kidogo.
Lakini lililowazi ni kwamba tumeona kuwa mfumo huu hauna muda mrefu nchini na unalengo la kumlinda mkulima wa Tanzania. Basi yatupasa kutupia jicho hizo changamoto zinazoletwa na wapinzani wa stakabadhi ghalani pia tutatoa maoni yetu jinsi ya kuzikabili na kuona mifano halisi ya mafanikio ya stakabadhi ghalani si Tanzania tu pia katika nchi za Ulaya Mashariki ambako mfumo huu unatumika pia.
Subscribe to:
Posts (Atom)