Monday, April 20, 2009

Mabilioni ya 'JK' yamekosea njia

Habari za manung'uniko ya wafanyabiashara wadogo wadogo na wajasiriamali zinasikika nchi nzima na kupamba magazeti ya kila siku na habari katika televisheni. Katuni nazo zinachorwa kuonesha kinacho wakumba wananchi wa Tanzania juu ya kile walichoahidiwa na Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika mapango wa kuwawezesha watu masikini nchini katika kujipatia mikopo ili kujikwamua na hali ngumu ya maisha.

Ni wazi kuwa nia ya fedha za 'JK' ni nzuri ila awamu hii tena ingawa Rais anajua na watanzania wengi wanajua kuwa Benki si rafiki wa watu masikini lakini ndiyo wamepewa mabiloni hayo wayasimamie. Sijui ni nini kimefanya fedha hizi zilizo na ni ya kuwainu watu masikini zipelekwe benki ya CRDB na NMB huku ukweli huo juu ya masharti magumu ukiwa wazi kwa kila mtu pamoja na JK mwenyewe!

Hakuna anayeweza kusema ni watu wangapi mpaka sasa wameweza kukopa kwani takwimu zinazotolewa zinaonesha wazi kuwa masharti yamewashinda wakopaji walio wengi.

Rai za wahariri wa magazeti mbalimbali nchini yamewahi kujoji na yanaendelea kuhoji juu ya nani hasa alikuwa anastahili kupata mkopo huu. Hakuna anayetoa jibu kati ya wahusika wakuu yaani Serikali na Benki zenye dhamana ya kusimamia mabilioni hayo.

Kinachoonekana sasa ni kuwa wenye nacho ndiyo watakao ongezewa. Yaani hao watu katika waombaji idadi ya maelfu kupata watu wasiozidi ishirini katika tawi la NMB Bukoba ni ushahidi kuwa wakopaji waliowengi hawawezi kuyafikia mabilioni haya.

Mkoani Tanga vyombo vya habari wiki iliyopita viliripoti juu ya kuvunjika kikao kufuatia wawakilishi wa benki kukosa majibu ya hoja kadhaa toka kwa wajumbe wa chama mkoani humo waliotaka kufahamu juu ya muenendo wa ukopeshaji.

Sasa jamii ya kitanzania hailewei kulikoni? Hasa watu masikini waliokuwa wameweka tegemeo lao katika mabilioni haya ya JK. Ni wazi kuwa mabilioni haya si sadaka na ni lazima yalindwe ili kuhakikisha yanarudi tena ili kuweza kukopesha wengine.

Ila Benki hazikustahili kupewa dhamana ya kuendesha mkopo huu.Makala haya itajaribu kuonesha ni kwanini tunasema Benki kupewa mabilioni ya JK ni kukosea njia.

Mkopaji awe mdogo au mkubwa si tu hukopa sehemu yoyote ile bali ile aliyoizoea. Mfano mzuri ni wewe mwenyewe msomaji wangu nina hakika umewahi kukopa hivyo basi katika kukopa kwako haujawahi hata siku moja kukopa iwe bidhaa au huduma mahali usikowahi kununua hata siku moja.

Hicho ndicho kinachotokea kila siku kwa wafanyabiashara,ukimueleza kama ataweza kukukopesha atakwambia we si mteja wangu. hapa maana yake ni kwamba kama angekuzoea na mazoea hayo ni kuwa uwe unapata huduma kwake ndipo ataweza kukuamini.

Sasa Benki nchini si wakopeshaji wa watu masikini na watu wasio na dhamana leo hii unapowapa taasisi hizi ambazo hawajazoea kidili na watu masikini utegemee nini kama siyo watu wengi kunyimwa mikopo hiyo kama hali inayotokea sasa. Hili liko wazi.

Tusidanganyike na majina kwani kuitwa national Microfinance Bank, si wekli kuwa inajihusiha na watu masikini hata kidogo.

Ni wazi kuwa Benki hizi hazina uzoefu wa kujihusihsa na watu wenye mitaji midogo na hasa masikini.Hivyo basi kukosa uzoefu huu kumewafanya wawe mwiba wakati wote.

Inawezekana kuwa wao si wabaya lakini NMB na CRDB wangekuwa tu wakweli na waungwana kwa kukataa kundesha zoezi hili kwani ni wazi kuwa wao hawana mazoea ya kukopesha watu amsikini hili liko wazi.Sasa sijui ni nini kimewafanya waje katika kona ambayo wao hawana uzaoefu nayo?

Tazania kuna taasisi zenye uzoefu wa kukopesha watu wenye kipato kidogo. Lakini safari hii hawakuwpewa nafasi hii.Binafsi nina amni kwani tafiti mablimbalim zilizofanywa zinaonesha ataasisi hizi za kibanafsi ziznfanya vizuri na zinamulekeo kweli ule wa Grameen Benki ya Profesa Mohammed Yunus mshindi wa tuzo ya Nobel na raia wa Bangladesh.

Taasisi hizo nim akama PRIDE(T),SEDA,MEDA,FINCA na FEDA kuzitaja kwa uchache.lakini pupa ndiyo tuakpeleka mbalioni NMB na CRDB huku tukijua wzi kuwa si rafiki wa masikini.

Taasisi hizi zinzendesha shughuki zake karibia nchi nzima na mahali kote zinafanya kwa ufanisi has katika kuota mikopo kwa watu wenye kipato kidogo ambao ndiyo walemngwa wa mkopo wa JK.

Profesa wa Uchumi Leonard Shio na Divina Shio katika tafiti yao; Institutions and Performance of Micro Enterprise in Tanzania,ilibaini kufanya vizuri kwa PRIDE(T),MEDA,SEDA,FEDA katika miko ay Mbeya,Arusha na Moerogoro na wakopeshwaji walikuwa ni wafanya bisahra wadogo. Mabo elo hii wanapigwa dnadana na NMB na CRDB.Ekwli wa mabo ni9 kuwa Benki hizi hazina uzoefu wa kujihushishan an kutoa mikopo kwa waut masikini isipokuwa wamaedandia tu!

Tafiti fualani iliyyofanywa na Mhadhiri mwandamizi wa Chuo Kikuu Mzumbe Josephat Itika aktika mji wa Morogoro ikihusianisha ushiriki wa wa Pride aktika kutoa amikopoo ana ukuaji wa ujasriamali,ilibaini kuwa PRIDE wana uwezo mkubwa wa kukusanya marejesho kwa zaidi ya 90% huku ikijikita kuwawezesha zaidi watu walio na kipato cha chini.

Lenye kutia moyo zaidi ni kuwa wakopaji wengi walikuwa ni akinam mama kwa zaidi ya 54%. Ni wazi kuwa mabilini haya ya JK kwa sasa yanatoka bila hata kujali usawa wa jinsia kitu ambco ni hatari.

SEDA(Small Enterprise Development Institute) ambayo ipo zaidia aktika mikopo aya kasiakazini mwa nchi mkoai Arshu pekee iliweza kukopesha watu zaidi ya 3000 wengi wao ndiyo hao Rais aliwalenga.

Pai taasisii hizi hutoa elimu kabla ya kutoa mikopo kwa wakoapji wake; juu ya namana ya kunedesha biashara kwa mafano PRIDE wana taasisi inayoitwa REDI. Ni wazi kuwa kama kusingekuwa na 'ushabiki' taasisi hizi zingekuwa ni za kupewa kundesha mkopo badala ya ahali ilivyo sasa.

NI wazi kuwa CRDB na NMB si taasisi zilizo na uzoefu wa kudili na watu wenye kipato kidogo. hatujachelewa kwani hadi sasa ni bilino 11 tu ndyo zimengizwa katika Benki hizo,na ni kiasi kidogo tu kimetoka. Ni bora kama tukiwapa kazi hiyo hizi taasisi zenye uzoefu wa kujishighulishs na watu masikini kama kweli tuna nia ya kuona umasikini wa kipato unapungua nchini.Na taasisi hizo ni PRIDE,MEDA,FEDA na zinginezo kuliko hali ilvyo sasa ya kuona tu mchezo wa maigizo.

Tukijipanga inawezekana kuwapa mitaji watu masikini lakini si kwa kupitia CRDB wala NMB.

No comments: