Monday, October 19, 2009

Uchawi na mafanikio ya biashara katika Tanzania

JE UNAAMINI KAMA UCHAWI UPO?
Gazeti la Mwananchi la tarehe 17 Oktoba, 2009 lina habari ya 'tafrani' katika kiwanda cha JUISI NA MAJI cha MOHAMMED ENTERPRISES kuhusu madai ya 'UCHAWI' dhidi ya Meneja wa kiwanda hicho. Ingawa gazeti halikutaja jina la Meneja, lakini yatupasa kufahamu kuwa kuna jambo kama hilo.
Polisi iliwalazimu kutumia silaha za moto kutawanya wafanyakazi, ni wazi kuwa walichoshwa na hali hii. Madai yao ni kwamba mara zote wamekuwa wakitolewa 'kafara' wafayakazi na wamekuwa wakikumbwa na ugonjwa wa 'kuanguka'.
Kiwanda cha 'OLAM', Mtwara kinacho bangua Korosho matatizo kama haya ya kuanguka kwa wafanyakazi yaliwahi kuripotiwa na kuna wakati 'makumi' waliumia baada ya kukanyagana wakihisi kuna 'dubwana', linawafuata KUWAMALIZA.
Ndiyo hizi ni siku za kafara, na kuabudu katika 'MIUNGU' inayohitaji 'DAMU' kama kafara ili kujiongezea kipato.Katika Biblia neno 'UCHAWI' limetajwa toka enzi za MUSA, YESU na MITUME walikuwa wakikemea kuhusu kushiriki katika UCHAWI.Kitabu kitakatifu cha Biblia kinasema wazi kwamba 'Usimuache mwanamke MCHAWI aishi, je wanawake ndiyo wachawi tu?
Inawezekana kwa namna moja au nyingine kuna wakati ulishindwa kuelewa kama kweli uchawi upo! Na kuna wakati ulikutana na watu wakisema kuwa hawaamini kama uchawi upo. Hata maoni yako yawe nini, suala moja unalopaswa kufahamu ni kwamba UCHAWI upo.
Lililowazi ni kwamba UCHAWI ni nguvu za yule muovu 'SHETANI'. Biblia inasema 'DUNIA' yetu i uwanja wa huyo muovu. La kumbe, tupo katika mji wa muovu, basi ni wazi kuwa UCHAWI unatuzunguka na wao wanataka kutushinda ili tuamini katika 'kushiriki' nao.
Basi kama binadamu yakupasa kuishi maisha yenye neema na kumtumikia 'MUNGU' wako, lakini unaweza kujiuliza kama MUNGU, anakupenda iweje akulete katika Uwanja wa 'SHETANI'?

Fuatilia makala haya itakayotoka hivi karibuni.

No comments: